Monday, July 14, 2014

Hivi ndivyo ilivyokuwa katika mchezo wa fainali kombe la dunia Ujerumani Vs Argentina: Habari Picha

Like ...

Mario Gotze apeleka furaha iliyokosekana Ujerumani takribani miaka 24

Na Fredrick Majula Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Buyern Munich Mario Gotze ameibuka shujaa wa taifa la Ujerumani baada ya kuipatia timu yake ya taifa ubingwa wa dunia kwa goli pekee alilofunga dhidi ya Argentina katika mchezo wa fainali uliyofanyika katika uwanja wa Maracana mjini Rio de Janeiro...

Wednesday, July 9, 2014

Huyu ndiye mfungaji mwenye magoli mengi zaidi katika historia ya fainali za Kombe la Dunia "Mjerumani, "Miroslav Klose" Avunja rekodi ya Ronaldo De Lima wa Brazil

Miroslav Klose amevunja rekodi ya Ronaldo na kuwa mfungaji mwenye mabao mengi zaidi katika historia ya fainali za kombe la dunia. Mshambuliaji huyo wa Ujerumani alifunga bao la pili katika ushindi wa mabao 7-1 dhidi ya Brazil kwenye mchezo wa nusu fainali wa kombe la dunia  na kufikisha mabao...

Hiki ndicho alichokisema Kocha wa Brazil Luiz Felipe Scolari baada ya kipigo cha 7-1 toka kwa Wajerumani

“Ni wakati mbaya zaidi kuwahi kutokea katika kazi yangu ya ukocha na siku mbaya zaidi katika maisha yangu ya soka. Lakini maisha yanaendelea. Nani anawajibika kwa matokeo haya? Ni mimi, ni mimi. Lawama za matokeo haya mabaya zinaweza kutuhusisha wote, lakini mtu aliyeamua timu ya kucheza na...