Wakati wimbi la kisiasa likiwachukua wasanii wengi wa Tanzania kutoka tasnia ya muziki na wale wa maigizo( Bongo Movie), nchini Nigeria imekuwa tofauti kwa msanii wa maigizo nchini humo Ramsey Noah, ambaye pia ni staa wa movie ya Kibongo The Devil Kingdom aliyoshirikishwa na Marehemu Stevene Kanumba. Akizungumza na mtandao wa NET Nouah amekaririwa akisema kuwa
yuko tofauti kabisa na wasanii wenzake wa nchini humo wanaokimbilia kwenye siasa kila kukicha na kuongeza kuwa mashabiki wake wasitegemee Ramsey kujiunga na siasa.
Akifanyiwa
mahojiano maalum na mtandao wa NET wa nchini humo, Ramsey alisema kuwa:
‘Sijui jinsi gani naweza kuwa mwanasiasa, mimi sio mwanadiplomasia
kivile. Sijui namna ya kuyapangilia maneno yakafana kama wanasiasa
wanavyoweza kufanya. Mimi siko hivyo’.
Source: NaijaGists.com
0 comments:
Post a Comment