Sunday, June 29, 2014

Mario Alberto Kempes : Shujaa aliyeiletea heshima Argentina Kombe la Dunia Mwaka 1978


Mchezaji mwenye rekodi ya pekee : Hakuwahi  kupewa kadi ya aina yeyote katika maisha yake ya soka                                         

Na Fredrick Majula

ContiSoccerWorld, Conti, Continental Tires, Tyres, Soccer, Football, World Cup, WC, 2010 FIFA World CupTM, Germany, Sponsoring, German Engineering, Conti Stars, WC Tickets, World Cup Tickets, Tickets, FIFA Partner 
Mara nyingi ukiizungumzia Argentina katika ramani ya soka ulimwenguni, wengi wanaamini ujio wa Diego Almando Maradona mwanzoni mwa miaka ya themanini ndio uliiweka nchi hiyo katika ramani ya soka kulingana na mchango wake katika timu ya taifa ya Argentina. Kabla ya kuibuka kwa Maradona tayari argentina walikuwa wameshatwaa kombe la dunia mwaka 1978, kipindi wanachukua kombe hilo, walikuwa na nyota wao ambaye aliibuka miaka ya sabini Mario Alberto Kempes, alizaliwa July 15, 1954 katika mji wa Bell Ville, Cordoba, Argentina.


 Kempesi alianza safari yake ya soka la kujulikana katika klabu ya Instituto de Cordoba mwaka 1973 ambayo aliichezea msimu mmoja tu na baadae kujiunga na klabu ya Rosario Central msimu uliofuata ambayo aliichezea kwa misimu miwili kutoka 1974-76, na kuifungia jumla ya magoli 100 ndani ya misimu miwili. Msimu wa 1976/77 nyota ya Kempes iling’aa hadi nchini Hispania ambapo Klabu ya Valencia iliweza kumsaini mshambuliaji huyo, ni hapo ambapo mafanikio yake katika ngazi klabu yalionekana kwani aliweza kutwaa vikombe viwili vya ligi ya Hispania, vikombe viwili vya Kombe la washindi barani ulaya pamoja na kikombe kimoja cha klabu bingwa barani ulaya. Pia katika misimu miwili mfululizo  Kempesi aliibuka mfungaji bora wa ligi ya Hispania akiwa kafunga jumla ya magoli 24 msimu wa 1976/77 na ule wa 1977/78 alifunga jumla ya magoli 28.

Mario Kempesi aliitwa kuchezea kikosi cha timu ya taifa ya Argentina kwa mara ya kwanza mwaka 1973 akiwa na umri wa miaka 19 tu katika mechi za kufuzu kombe la dunia la mwaka 1974. Katika kukitumikia kikosi chake cha timu ya Taifa, Kempesi alifanikiwa kucheza michuano 3 ya kombe la dunia ikiwemo ile ya 1974, 1978 na ile ya 1982. Katika fainali hizo tatu ni michuano ya mwaka 1978 ndio ilimuweka Kempes pamoja na Argentina katika historia ya kuitwa bingwa wa kombe la dunia baada ya kushinda mchezo wa fainali dhidi ya Uholanzi kwa jumla ya magoli 3 kwa 2 ya Uholanzi huku Kempes akifunga magoli  mawili katika ushindi huo, na kupoza kiu ya miaka mingi kwa Argentina, ambayo haikuwahi kutwaa ubingwa wa kombe hilo tangu michuano hiyo ianze mwaka 1930.


Pia katika michuano Mario aliibuka mshindi wa kiatu cha dhahabu. Katika Safari yake ya  soka la kimataifa Mario Kempesi ni mchezaji ambaye hakuwahi kuoneshwa kadi ya njano wala kutolewa uwanjani kwa kadi nyekundu mpaka kustafu kwake soka mwaka 1996. Kwa sasa Mario Kempes ni mchambuzi wa michezo katika kituo cha televisheni ESPN.

0 comments:

Post a Comment