Sunday, October 12, 2014

Sudan yawaibisha mabingwa wa Afrika


Wachezaji wa Nigeria
Mabingwa wateteza wa kombe la taifa bora barani Afrika Nigeria walishangazwa Ugenini baada ya kuchapwa bao moja kwa bila na Sudan na hivyobasi kusalia mkia katika kundi A la michuano ya kufuzu kwa faibnali za dimba hilo.
Bao la Bakri Almadina dakika chache tu kabla ya kipindi cha kwanza kukamilika lilitosha kuiwezesha Sudan kushinda mchuano huo.
Kikosi cha Super Eagles chini ya Ukufunzi wa Stephen Keshi kilihitaji ushindi katika mechi hiyo ili kuanzisha kampeni yake ya kufuzu,baada ya kushindwa na Congo Brazaville na kutoka sare na Afrika kusini .
Katika Matokeo ya mechi zengine:
Malawi 0-2 Algeria
Uganda 0-1 Togo
Ethiopia 0-2 Mali
Mozambique 2-0 Cape Verde
S Leone 0-0 Cameroon
Congo 0-2 South Africa
DR Congo 1-2 Ivory Coast
Niger 0-0 Zambia
Sudan 1-0 Nigeria
Gabon 2-0 B Faso
Guinea 1-1 Ghana

UN:Ebola kudhibitiwa kwa miezi mitatu



David Nabarro

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayehusika na ugonjwa wa Ebola David Nabarro ameiambia BBC kuwa mlipuko wa ugonjwa huo magharibi mwa Afrika unaweza kudhibitiwa katika kipindi cha miezi mitatu.
Dr.Nabarro alisema kuwa ina maana kuwa visa vipya vya ugonjwa huo vitapungua kila wiki.
Amesema kuwa kwa sasa maambukizi ya ugonjwa wa Ebola ni ya juu hata baada ya kuwepo kwa jitihada za kimataifa.
Nabarro amesema kuwa kuuelewa ugonjwa wa Ebola miongoni mwa jamii zilizoathirika kutasaidia kupambana nao kwa kuwa watu wanaelewa kwamba kuwatenga wagonjwa ndiyo njia bora ya kuzuia maambukizi.
Zaidi ya watu 4000 wameaga dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola wengi kutoka mataifa ya Sierra Leone, Liberia na Guinea.

Friday, October 10, 2014

Hong kong bado hapakaliki

WANAFUNZI: MAANDAAMANO BADO HONG KONG

Waandamanaji Hong Kong
Serikali ya eneo la Hong Kong imeitisha mazungumzo maalumu na viongozi wa wanafunzi ambao wamekuwa wakiratibu maandamano yaliyodumu kwa wiki mbili hadi sasa.
Mkutano huo wa serikali ya eneo hilo na wanafunzi unatarajiwa kufanyika leo.waandamanaji hao wanapinga utawala wa Beijing kuwachagulia mgombea katika uchaguzi mkuu wa eneo hilo 2017.
Hata hivyo wanafunzi hao wamesisitiza kuwa wataendelea na mgomo huo pamoja na serikali hiyo kuhitaji mazungumzo na viongozi wao.
Waandamanaji hao kwa sasa wamekuwa wakiendelea na maandamano huku baadhi ya huduma mhimu na kazi zikidorola.BBC

England yang'ara kwa vibonde San Marino

YAISAMBARATISHA SAN MARINO 5-0
Timu ya England imefanikiwa kupata ushindi mara mbili katika michezo miwili ya kundi E ya kufuzu kucheza michuano ya bara la Ulaya ya mwaka 2016 baada ya kupata ushindi mnono wa 5-0 dhidi ya San Marino.
England alianza kuvuna magoli kupitia kwa mlinzi wake Phil Jagielka aliyefunga katika dakika ya 24 kwa mpira wa kichwa kabla ya Wayne Rooney kuongeza bao la pili kwa njia ya penalti katika dakika ya 43 kutoka na madhambi ya mchezaji wa San Marino Andy Selva.
Naye mshambuliaji Danny Welbeck alifanikiwa kutumbukiza goli la tatu kwenye dakika ya 49. Goli hili lilitokana na mpira wa pasi kutoka kwa mchezaji mwenzake wa Arsenal ambaye aliingia kipindi cha pili Alex Oxlade-Chamberlain.
Andros Townsend aliiongezea timu yake ya England goli la nne kwa mkwaju wa mbali kabla ya Alessandro Della Valle kujifunga mwenyewe kutokana na kugongwa na mpira uliopigwa na Rooney.
Matokeo ya michezo mingine: Belarus 0: Ukaraine 2, Macedonia 3: Luxembourg 2, Slovakia 2: Spain 1, Lithuania 1:Estonia 0, Slovenia 1: Switzerland 0, Liechtenstein 0: Montenegro 0, Moldova 1:Austria 2, Sweden 1: Russia 1 BBC

Hivi ndio vichwa vya habari za magazeti ya leo October 10 2014




.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

T.shirt ya maneno ya Kiswahili aliyovaa Seneta wa Nairobi ''Sonko'' ikiwatusi ‘wazungu’ 

UH 2Mike Sonko ni yule Mwanasiasa mwenye vituko ambae alipata umaarufu sana toka akiwa mbunge kwa kuwa na swagg zake kivyakevyake, alikua mbunge kijana ambae anaingia na hereni bungeni, blingbling kibao kama cheni na pete kama anavyoonekana ametupia kwenye hii picha hapa juu akiwa sasa ni Seneta wa jiji la Nairobi.

Hiki ni kiasi cha fedha walizotumia Barcelona kuwaleta marafiki Neymar kwenye utambulisho wake
Screen Shot 2014-10-10 at 9.16.37 AM
Usajili wa kumleta Neymar Dos Santos katika klabu ya FC Barcelona uligubikwa na utata mkubwa na hatimaye ulimgharimu Sandro Rosel kazi yake ya urais katika klabu hiyo ya Catalunya.