Friday, October 31, 2014

Kiwango cha kalori katika pombe kitajwe

Wataka pombe ionyeshe kiwango cha kalori kupunguza vitambi na unene wa kupitiliza

Pombe inatakiwa kuwa na nembo inayoonyesha kiwango cha kalori au kipimo cha joto litolewalo na chakula ili kupunguza vitambi au unene wa kupita kiasi.
Madaktari wa afya ya umma, wameonya kuwa glasi kubwa ya mvinyo inaweza kuwa na kiasi cha kalori 200- sawa na donati, aina ya maandazi.
Hata hivyo idadi kubwa ya watu hawajui madhara ya kula kiwango kikubwa cha kalori.

Waziri wa Afya Jane Ellison amesema "hatua kubwa" imefanyika kwa kuviwekea nembo vyakula, na kwa suala hilo serikali italiangalia.
Sekta ya vinywaji imesema imesema iko tayari kwa wazo hilo la kuweka nembo zenye kuonyesha kiasi cha kalori, lakini kuweka nembo zinazonyesha kiwango cha kilevi katika kinywaji ni muhimu zaidi.

Sunday, October 19, 2014

Maji ya kuosha wafu,kivutio cha biashara


mortuary

Katika tukio la kushangaza na la kutaka kujiongezea mapato pamoja na kushamiri kwa biashara,wafanyibiashara wawili katika mtaa wa Lobengula nchini Zimbabwe walizozania maji machafu yanayopatikana baada ya kuosha wafu ambayo huyatumia kuvutia wateja.
Kwa mujibu wa BBC, Wawili hao waliojulikana kama ViolaTshuma na Molene Hadebe walikabiliana vilivyo baada ya Hadebe kuchukua kiwango kikubwa cha maji hayo ya kuosha maiti kabla ya mwenzake kuwasili.
Wafanyibiashara hao wanaodaiwa kuwa rafiki wakubwa walipata maji hayo kutoka chumba kimoja cha mazishi katika mji wa Bulawayo kwa biashara yao ya kila siku.
Kulingana na wafanyibiashara wengine maji hayo huuzwa kwa wafanyibishara na wanawake wanaotumia kufanya tambiko.
Maji hayo pia hutumika kuwazima wanaume walio wakali kwa wake zao baada ya kubaini kwamba wake hao wanawanyemelea wanaume wengine.
Wafanyibiashara waliohijiwa pia walibaini kuwa maji hayo pia hutumiwa kuosha matunda na hata nyanya ili kuwavutia wateja wengi kama wale wanaouhudhuria mazishi.

Wakatoliki wakataa kuwatambua mashoga.



Ndoa ya mashoga

Makundi ya kikatoliki yanayopigania haki za wapenzi wa jinsia moja yameelezea ghadhabu yao kutokana na hatua ya maaskofu wa kanisa hilo ya kukataa mapendekezo ya kutangaza msimamo kuhusu mashoga, wasagaji pamoja na watu waliotalakiana na wanaoana.
Wakati wa kumalizika kwa mkutano wa maaskofu wa kanisa katoliki, Vatican ilishindwa kupata theluthi mbili ya kura za maskofu wa kuunga mkono maoni yao kuhusu masuala hayo.
Kundi la kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja nchini Marekani la New Ways Ministry limesema kuwa hatua ya maskofu hao kuamua kujadili suala hilo ni matumaini ya siku za usoni.
Masuala hayo yanatarajiwa kuzungumziwa tena baada ya mwaka mmoja.*BBC Swahili*

Hizi ni nukuu za mapenzi kutoka kwa watu maarufu duniani october 19, 2014


Bob Marley

“Only once in your life, I truly believe, you find someone who can completely turn your world around. You tell them things that you’ve never shared with another soul and they absorb everything you say and actually want to hear more. You share hopes for the future, dreams that will never come true, goals that were never achieved and the many disappointments life has thrown at you.

 When something wonderful happens, you can’t wait to tell them about it, knowing they will share in your excitement. They are not embarrassed to cry with you when you are hurting or laugh with you when you make a fool of yourself. Never do they hurt your feelings or make you feel like you are not good enough, but rather they build you up and show you the things about yourself that make you special and even beautiful. There is never any pressure, jealousy or competition but only a quiet calmness when they are around. You can be yourself and not worry about what they will think of you because they love you for who you are. 

Friday, October 17, 2014

Hiki ndicho kilichowahi kutokea katika tarehe kama ya leo octoba 17, miaka mingi iliyopita

History logo
Miaka 41 iliyopita katika siku kama hii ya leo nchi za Kiarabu zinazouza nje mafuta zilianza kutekeleza vikwazo vya mafuta dhidi ya Marekani, Uingereza na makampuni yanayouuzia mafuta utawala wa Kizayuni wa Israel. Hatua hiyo ilichukuliwa kutokana na uungaji mkono mkubwa wa Marekani na Uingereza kwa utawala ghasibu wa Israel katika vita vya Israel dhidi ya Syria na Misri. Hatua hiyo ilipandisha sana bei ya mafuta katika masoko ya kimataifa na kutoa pigo kubwa kwa nchi hizo za Magharibi. Muda mfupi baadaye nchi za Kiarabu zilikiuka vikwazo hivyo vya mafuta na kuanza tena kuiuzia mafuta Marekani na Uingereza. Vikwazo hivyo vilionesha kuwa nchi za Kiislamu zina silaha muhimu inayoweza kutumiwa dhidi ya uungaji mkono mkubwa wa nchi za Magharibi kwa utawala katili wa Israel.

Na Siku kama ya leo miaka 31 iliyopita, aliaga dunia mtaalamu wa masuala ya jamii wa Kifaransa kwa jina la Raymond Aron. Aron alizaliwa mwaka 1905. Msomi huyo wa Kifaransa alikuwa akifundisha pia taaluma hiyo ya masuala ya jamii katika Chuo Kikuu cha Sorbonne, Paris kwa miaka kadhaa. Vilevile alikuwa akiandika makala katika majarida ya Le Figaro na Express mjini Paris. Raymond Aron ameandika vitabu vingi na hapa tunaweza kuashiria vitabu vyake vichache alivyovipa majina ya "Kuanza Vita vya Nyuklia, "Mapambano ya Kitabaka" na "Miaka ya Mwishoni mwa Karne".