Saturday, September 5, 2015

Ebola yatatiza tena Sierra Leone


Watu 1,000 nchini Sierra Leone wamewekwa kwenye karantini baada ya kugunduliwa kuwa mwanamke wa umri wa miaka 67 alifariki kutokana na Ebola.
Hilo limejiri siku tano tu baada ya kuanza kwa hesabu ya wiki sita iliyolenga kutangaza taifa hilo kuwa bila Ebola.

 Maafisa wa kukabili Ebola


Karantini hiyo itadumu wiki tatu, mradi tu kusiwe na visa vipya vitakavyoripotiwa.
Watu Zaidi ya 11,000 wamefariki tangu kuanza kwa mkurupuko wa Ebola nchini Sierra Leone, Guinea na Liberia.Maafisa wa serikali nchini humo walikuwa na matumaini baada ya kupita kwa kipindi kirefu bila kisa kipya cha Ebola na kwamba kisa cha sasa kimewashangaza.
Mwandishi wetu anasema karantini ya sasa ina masharti makali zaidi kuliko za awali. Ni pamoja na amri ya kuzuia watu kutembea kutoka nyumba moja hadi nyingine.
Wanajeshi na maafisa wa polisi wametumwa kudumisha karantini hiyo katika kijiji cha Sellakaffta, kilichoko Kambia kwenye mpaka wa kaskazini wa taifa hilo na Guinea.
Maafisa wa Shirika la Afya Duniani na wizara ya afya Sierra Leone wanapanga kutoa chanjo kwa wale ambao huenda walikutana na mwanamke huyo.
Guinea inajaribu kudhibiti mkurupuko wa ugonjwa huo nchini humo. Liberia, WHO ilitangaza kuwa virusi vya Ebola vimeacha kusambaa kwa mara ya pili Alhamisi.
Taifa hilo lilitangazwa kutokuwa na Ebola mwezi Mei lakini visa zaidi vikaripotiwa mwezi uliofuata.
SOURCE:BBC SWAHILI.

Related Posts:

  • Saudia yaamuru kuungwa mkono magaidi Wizara ya Mwongozo na Wakfu ya Saudi Arabia imewataka mahatibu misikitini  kuyaungwa mkono makundi ya kigaidi. Taarifa iliyotolewa leo na wizara hiyo imeeleza kuwa, makhatibu wa misikiti nchini humo wameta… Read More
  • Stages of Surrender I have to confess that I used to suffer from a very significant disease. You might not have noticed it by looking at me, but if you had lived with me for awhile you probably would have. It has a very special name, and it’s … Read More
  • UN:Ebola kudhibitiwa kwa miezi mitatu David Nabarro Mjumbe wa Umoja wa Mataifa anayehusika na ugonjwa wa Ebola David Nabarro ameiambia BBC kuwa mlipuko wa ugonjwa huo magharibi mwa Afrika unaweza kudhibitiwa katika kipindi cha miezi mitatu. Dr.Nabarro al… Read More
  • Sudan yawaibisha mabingwa wa Afrika Wachezaji wa Nigeria Mabingwa wateteza wa kombe la taifa bora barani Afrika Nigeria walishangazwa Ugenini baada ya kuchapwa bao moja kwa bila na Sudan na hivyobasi kusalia mkia katika kundi A la michuano ya kufuzu kwa faib… Read More
  • 13 Simple Tricks To A Long And Happy Marriage It's no secret that marriage takes work. After all, we're only human, and humans make mistakes, have bad days and sometimes even forget to load the dishwasher (again). Nevertheless, some couples are able to foster happy,… Read More

0 comments:

Post a Comment