Msemaji wa shirika la msalaba mwekundu katika eneo la Lamu na
Kilifi Bwana Musa Hassan, ameliambia gazeti la The Standard kuwa
asilimia kubwa ya watu wanaotoroka ni wakaazi wa eneo la Basuba na
wengine walioko Kusini mwa Garissa wanaohofia kupatikana katikati ya
makabiliano yanayotarajiwa kati ya wanamgambo hao na vikosi vya usalama
vya Kenya.
Wizara ya usalama ilitoa ilani mwishoni mwa juma
ikiwataka wakaazi wa maeneo yanayopakana na msitu huo ikiwataka watu
wote wanaomiliki bunduki katika eneo hilo kuzisalimisha kabla ya kuanza
kwa operesheni hiyo inayohusisha vikosi vya wanahewa na wale wa nchi
Kavu.
Tayari idadi kubwa ya vikosi vya jeshi vimeripotiwa
kuonekana katika maeneo ya Mangai, Baure,Kaskazini mwa Lamu, Bodhai na
Hulugho.
Mkuu wa polisi katika eneo la Ijara Christopher Rotich
amenukuliwa akithibitisha kuwepo kwa mipango hiyo ya kudhibiti utovu wa
usalama unaotokana na mashambulio ya mara kwa mara yanayodaiwa
kutekelezwa na kundi hilo la wanamgambo la wa Jeysh al Ayman.
Kundi hilo lanalosemekana kujumuisha wenyeji linalaumiwa kwa jaribio la kuvamia kambi ya kijeshi iliyoko Baure mwezi juni.
Aidha kundi hilo ndilo linalodaiwa kutekeleza shambulizi la bomu la kutegwa ardhini mapema mwaka huu.
Majuzi tu kundi hilo linadaiwa kuvamia wanakijiji wa
Basuba na kutoa hutuba kwa muda mrefu mbali na kuwaonya wenyeji dhidi
ya kutoa habari na kushirikiana na polisi.
Inspekta mkuu wa polisi
wa Kenya, Joseph Boinnet, alitangaza hali ya tahadhari katika maeneo ya
msitu wa Boni huku akitoa amri ya kuitangaza Boni kuwa eneo la
Operesheni.
Msitu huo mkubwa wa Boni upo katika majimbo tatu nchini Kenya ya Lamu, Garissa na Tana River.
Aidha unapakana na bahari Hindi kuanzia Lamu hadi mpaka wa Kenya na Somalia.
SOURCE: BBC SWAHILI
0 comments:
Post a Comment