Saturday, September 5, 2015

Kikwete: Uwajibikaji utasaidia maendeleo ya Afrika

    kuzisha hati

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema mapema leo kuwa, uwazi na uwajibikaji utasaidia kuharakisha maendeleo barani Afrika. Rais Kikwete amesema hayo wakati wa kufungua rasmi mkutano wa takwimu huria barani Afrika ulioanza leo jijini Dar es Salaam. Kwenye hotuba yake Rais Kikwete amesema kuwa, serikali za Afrika zinapaswa kuweka wazi takwimu zao ili raia wawe na ufahamu wa yale yanayofanywa na viongozi wao. Rais wa Tanzania amesema kufanya hivyo kutaondoa misuguano inayoshuhudiwa mara kwa mara kati ya raia na serikali hususan nyakati za matukio ya kisiasa kama vile uchaguzi mkuu au kura ya maamuzi.
Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na zaidi ya wajumbe 400 kutoka nchi kadhaa za Afrika wakiwemo wawakilishi wa serikali, sekta binafsi, wataalamu na wasomi pamoja na wawekezaji.
SOURCE: TEHRAN

0 comments:

Post a Comment