Saturday, September 5, 2015

Kikwete: Uwajibikaji utasaidia maendeleo ya Afrika

    kuzisha hati

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema mapema leo kuwa, uwazi na uwajibikaji utasaidia kuharakisha maendeleo barani Afrika. Rais Kikwete amesema hayo wakati wa kufungua rasmi mkutano wa takwimu huria barani Afrika ulioanza leo jijini Dar es Salaam. Kwenye hotuba yake Rais Kikwete amesema kuwa, serikali za Afrika zinapaswa kuweka wazi takwimu zao ili raia wawe na ufahamu wa yale yanayofanywa na viongozi wao. Rais wa Tanzania amesema kufanya hivyo kutaondoa misuguano inayoshuhudiwa mara kwa mara kati ya raia na serikali hususan nyakati za matukio ya kisiasa kama vile uchaguzi mkuu au kura ya maamuzi.
Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na zaidi ya wajumbe 400 kutoka nchi kadhaa za Afrika wakiwemo wawakilishi wa serikali, sekta binafsi, wataalamu na wasomi pamoja na wawekezaji.
SOURCE: TEHRAN

Related Posts:

  • Marekani yakiri mapambano ya mjini Kobani ni magumu Waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck Hagel amesema siku ya Jumamosi kuwa mji wa Syria wa Kobani ni tatizo kubwa na gumu, lakini mashambulizi ya angani yamepiga hatua katika kuwarudisha nyuma wapiganaji wa Dola ya Kiislamu. … Read More
  • Vichwa vya habari magazeti ya leo October 12 / . . . . . . . . . . , . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . … Read More
  • Saudia yaamuru kuungwa mkono magaidi Wizara ya Mwongozo na Wakfu ya Saudi Arabia imewataka mahatibu misikitini  kuyaungwa mkono makundi ya kigaidi. Taarifa iliyotolewa leo na wizara hiyo imeeleza kuwa, makhatibu wa misikiti nchini humo wameta… Read More
  • Wakili asema Pistorius 'amefilisika' Inaarifiwa Pistorius ametumia pesa zake kwa kesi inayomkabiliPistorius aliangua kilio wakili wake alipoambia mahakama kuwa amefilisika Mahakama inayosikiliza kesi dhidi ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pis… Read More
  • Stages of Surrender I have to confess that I used to suffer from a very significant disease. You might not have noticed it by looking at me, but if you had lived with me for awhile you probably would have. It has a very special name, and it’s … Read More

0 comments:

Post a Comment