Sunday, September 6, 2015

Al Shabab wateka miji miwili kusini mwa Somalia

 http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/fec01bb37336bdc554b56465a0fd13d5_XL.jpg
Magaidi wa kundi la al Shabab wamedai kuchukua udhibiti wa miji miwili kusini magharibi mwa Somalia siku chache tu baada ya kushambulia kituo cha vikosi vya Umoja wa Afrika katika eneo hilo.
Msemaji wa al Shabab amesema kundi hilo limeteka miji miwili midogo katika eneo la Lower Shabelle ambayo ni El Saliindi, yapata kilomita 65 kusini mwa Mogadishu na Kuntuwarey katika barabara ya Mogadishiu-Barawe.
Kaimu gavana wa Lower Shabelle, Ali Nur amethibitisha kuwa miji hiyo miwili imeanguka mikononi mwa al Shabab. Aidha leo Jumamosi magaidi wa kundi hilo la wakufurishaji wameshambulia msafara wa askari wa Umoja wa Afrika katika mji wa Marka huko huko Lower Shabelle na kudai kuwa wameua askari kadhaa. Septemba Mosi magaidi wa al Shabab walivamia kituo cha askari wa Umoja wa Afrika huko Janale yapata kilomita 90 kusini mwa Mogadishu na kuwaua askari 12 wa Uganda walio katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika.

SOURCE: Radio Tehran

0 comments:

Post a Comment