Waziri wa ulinzi wa Marekani Chuck Hagel amesema siku ya Jumamosi kuwa mji wa Syria wa Kobani ni tatizo kubwa na gumu, lakini mashambulizi ya angani yamepiga hatua katika kuwarudisha nyuma wapiganaji wa Dola ya Kiislamu.
Vikosi vya wapiganaji wa Kikurdi wanaoulinda mji huo wameutaka muungano unaoogozwa na Marekani kuzidisha mashambulizi ya angani dhidi ya wapiganaji wa IS ambao wamezidi kuuzingira mji huo wa Syria uliyoko mpakani na Uturuki siku ya Jumamosi.