Friday, April 24, 2015

Boko Haram labadilisha jina Nigeria

Kiongozi wa wapiganaji wa Boko Haram Abubakar Shekau
Picha mpya zimetolewa kuhusu wapiganaji wa Boko Haram ambao wanajielezea kuwa Islamic State Jimbo la Magharibi mwa Afrika.

Kundi hilo limekuwa watiifu kwa wapiganaji wa Islamic State mwezi uliopita.
Baadhi ya wanajeshi wa Nigeria ambao wameshirikishwa katika oparesheni ya kulishinda kundi hilo katika msitu wa Sambisa uliopo Kazkazini mashariki wamelazimika kurudi nyuma kwa kuwa wanadhani kwamba huenda msitu huo umewekwa mitego.
Mwanachama wa kundi moja la kuweka usalama mtaani JTF ameiambia BBC kwamba mwanajeshi mmoja na walinzi watatu wa mitaani waliuawa wakati gari lao lilipopita juu ya mtego.

0 comments:

Post a Comment