Shirikisho
la soka nchini Tanzania (TFF) limepitisha azimio la kila mchezaji wa
kigeni kulipa dola 2,000 ( wastani wa milioni 5) kwa kila msimu
atakaocheza ligi kuu ya Tanzania.
Kiasi hicho cha pesa kitaanza kulipwa katika msimu ujao wa ligi wa 2015/2016 .
Wachezaji
wa kigeni waliosalia kuendelea kuchezea timu zao na wale wanaosajiliwa
kwa ajili ya msimu ujao watalazimika kulipa kiasi hicho cha pesa.
Msemaji
na afisa habari wa TFF, Baraka Kizuguto amesema maamuzi ya kikao cha
kamati ya utendaji ya TFF kilichoketi Jumamosi visiwani Zanzibar ni kuwa
kiasi hicho cha pesa kitakuwa ni kwa ajili ya kuendeleza mpira wa miguu
nchini Tanzania.
Katika miaka ya nyuma, wachezaji wa kigeni
kutoka nchi mbalimbali, hasa za Afrika ya Mashariki, Kenya, Uganda,
Rwanda na Burundi walikuwa hawatozwi kiasi chochote cha pesa licha ya
kulipwa mamilioni.
Kizuguto amesema fedha hizo zitapelekwa katika mfuko wa maendeleo ya mpira wa miguu ujulikanao kama (Football Development Fund
Source: BBC Swahili
Source: BBC Swahili
0 comments:
Post a Comment