Dar es
Salaam. Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Joseph Warioba amewashangaa makada wanaojinadi kuwa ni wasafi na
waadilifu, akisema sifa hizo zinatakiwa zitolewe na jamii.
Jaji
Warioba, mmoja wa watu ambao wamekuwa wakikemea masuala ya ukiukwaji wa
maadili, pia amesema hatamuunga mkono mgombea ambaye anakiuka maadili ya
uongozi.
Tayari
makada 37 wamejitokeza kuomba ridhaa ya wana-CCM kugombea urais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wengi wao wamekuwa wakijinadi kuwa
ni wasafi na waadilifu na kuwataka wanachama kutowapitisha watu wenye
harufu ya ufisadi na wasio waadilifu.
Lakini Jaji Warioba alisema anaona wanakwenda kinyume na inavyotakiwa kufanyika.
“Viongozi
wa sasa wanaonekana hawajali misingi ya maadili kwa sababu jamii yetu
yenyewe imeonyesha kutochukizwa na suala hili la mmomonyoko wa maadili
na wala jamii haijalipa uzito unaostahili,” alisema Jaji Warioba wakati
wa uzinduzi wa kampeni ya Vuguvugu la uhuishaji wa Maadili kwa Jamii
(Moral Rivival Movement).
“Viongozi
wengi waliochukua fomu za kugombea urais wanaonekana kujitangaza kuwa
wao ni waadilifu. Jamii ndiyo ilipaswa kusema kuwa viongozi hao ni
waadilifu au sio waadilifu na sio wao kujinadi,” alisema Warioba ambaye
pia aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu.
Mkutano
huo ulioandaliwa na viongozi wa dini kwa kushirikiana na Chama cha
Wataalamu wa Wakikristo (CPT) ulijadili ujenzi mpya wa maadili katika
jamii utasadia kupata kiongozi mwenye misingi ya maadili ili kuepuka
mitafaruku baina ya siasa za madaraka na siasa za maslahi.
“Nimekuja
hapa leo (jana) kuwaunga mkono katika uzinduzi wa Vuguvugu la Uhaishaji
Maadili kwa Jamii kwa sababu na mimi ni sehemu ya mapambano hayo.
Sitaunga mkono ng’o kiongozi yeyote ambaye ataonekana kutokuwa na
misingi ya maadili ya uongozi katika kipindi hiki cha uchaguzi,” alisema
Jaji Warioba.
Warioba,
ambaye alieleza kuwa ameamua kukaa kimya kuhofia kila anachosema
kuhusishwa na masuala ya uchaguzi, alisema viongozi ambao hawana maadili
wamechangia kwa kiasi kikubwa kuwapo kwa mianya ya rushwa.
“Lakini
kama tunataka kuwa na viongozi wenye misingi ya maadili, ni lazima
tujenge upya maadili kwa sababu tusipofanya hivyo yatazidi kuporomoka,”
alisema waziri mkuu huyo wa zamani.
Azungumzia suala la ubaguzi:
“Tumeona
sasa ukabili umeanza kurudi, ubaguzi wa kidini umeanza kurudi, ubaguzi
wa kikanda umeanza kurudi, ubaguzi wa namna hii umeanza kurudi kutokana
na kukosekana kwa maadili,” alisema Jaji Warioba ambaye alitumia muda
mwingi kuishauri jamii kufuata misingi ya maadili iliyoachwa na
waasisi.Profesa Beda Mutagahywa anena:
Akizungumzia
maana ya Uhuishaji maadili( MRM), Profesa Beda Mutagahywa alisema ni
hamasa ya umma kwenda mbele kufikia malengo fulani ya kijamii na malengo
hayo yapo, yalikuwepo lakini hamasa ya kuyafikia ilififia na hatimaye
malengo yakasahaulika.
“Hii
itasadia kama tutafanikiwa kuufanya uwe ajenda na sehemu ya ilani ya
vyama mbalimbali vya siasa katika uchaguzi mkuu ujao,” alisema.Source: Mjengwa blog via Mwananchi
0 comments:
Post a Comment