Kiwango cha ushindani Ligi kuu ya Tanzania Bara kinatarajiwa kuongezeka na kufungua
milango zaidi kwa wachezaji wa kigeni baada ya vilabu kuruhusiwa
kusajili wachezaji 7 wa kigeni kuanzia msimu ujao wa ligi.
Awali,
baadhi ya vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara vilipendekeza
usajili wa wachezaji 10 wa kigeni lakini Shirikisho la mpira wa miguu
(TFF) limeamua ni 7 tu wanaweza kusajiliwa na kucheza kwa wakati wote.
Katika misimu iliyopita, kila timu iliruhusiwa kusajili wachezaji wa kigeni wasiozidi watano.
Hata
hivyo, si vilabu vyote vitaweza kusajili wachezaji wa kigeni kwa kuwa
na vyanzo vidogo vya pesa, bali vilabu vikubwa kama vile Simba,Yanga na
Azam vitaweza kumudu gharama za usajili
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF, mikakati ya kusajiliwa wachezaji hawa ni haya yafuatayo:
- Mchezaji awe ni mchezaji wa timu za Taifa za nchi yake kuanzia timu ya taifa au timu za vijana za U23, U20, U19 na U17.
- Mchezaji awe anacheza katika ligi kuu ya nchi yake au nchi nyingine wakati anasajiliwa.
Wimbi
la wachezaji wa kigeni linaongezeka nchini Tanzania baada ya ligi ya
nchi hiyo kuwa ni ligi yenye ushindani na vilabu kutoa pesa nyingi kwa
ajili ya usajili na mshahara.
Kwa habari zisizo rasmi, ligi ya
Tanzania Bara inasemekana ndio ligi inayoongoza katika ukanda wa Afrika
ya Mashariki kwa ushindani.
Source: BBC Swahili
0 comments:
Post a Comment