Magaidi wa kundi la al Shabab wamedai kuchukua udhibiti wa miji
miwili kusini magharibi mwa Somalia siku chache tu baada ya kushambulia
kituo cha vikosi vya Umoja wa Afrika katika eneo hilo.
Msemaji wa al Shabab amesema kundi hilo limeteka miji miwili midogo
katika eneo la Lower Shabelle ambayo ni El Saliindi, yapata kilomita 65
kusini mwa Mogadishu na Kuntuwarey katika barabara ya Mogadishiu-Barawe.