Wednesday, November 25, 2015

Kama wewe unatafuta ajira, taarifa hii kutoka Secretariate ya Ajira na Utumishi wa Umma Tanzania Inakuhusu

Maelekezo muhimu ya ujazaji wa Taarifa kwenye mfumo wa Recruitment Portal kwa waombaji kazi


 Sekretarieti ya ajira katika utumishi wa Umma imeanzisha mfumo wa kielektroniki wa utumaji wa maombi ya kazi (Recruitment Portal) ambao humsaidia muombaji kazi kutuma maombi hayo popote alipo ndani na nje ya Nchi kwa njia ya mtandao.
Ni muhimu kuzingatia kuwa kabla ya ujazaji wa taarifa kwenye mfumo wa ajira kila muombaji kazi lazima awe na barua pepe ambayo ni hai(Active email address) ambayo atatakiwa kujisajili katika sehemu iliyoandikwa Register katika ukurasa wa mbele wa mfumo (Home page) kabla ya muombaji kujaza taarifa zake katika vipengele 11 vilivyoelezewa kwenye makala haya. Pia kwa waombaji wote wanatakiwa kuhakikisha taarifa zao zote wanazojaza ni za uhakika na zipo katika ukamilifu.
 
Mfumo huu unapatikana kupitia anuani ya portal.ajira.go.tz ambapo baada ya usajili mwombaji kazi atajaza taarifa zake. Mgawanyo wa taarifa hizo upo katika vipengele vikuu 11 ambavyo ni Taarifa binafsi (Personal Details), Taarifa za Mawasiliano (Contact Details), Sifa za kielimu (Academic Qualifications), Sifa za Kitaaluma (Professional Qualifications), uwezo wa lugha (Language Proficiency), uzoefu wa kazi (Working Experience), Mafunzo, Warsha na Makongamano aliyowahi kuhudhuria (Training & Workshop Attended), ujuzi wa matumizi ya kompyuta (Computer Literacy), wadhamini (Referees), viambatanisho vingine (Other Attachments) na udhibitisho wa taarifa zilizoingizwa (Declaration). Aidha kila kipengele kinapaswa kujazwa kulingana na kinavyojieleza kwa ukamilifu wake.
Kwa kuwa kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya waombaji kazi kutojaza taarifa zao kikamilifu au kujaza baadhi ya taarifa zao kwenye vipengele visivyohusika, makala hii itajikita katika kuelezea kwa kina taarifa gani zinapaswa kujazwa kwa kila kipengele ili kuweka uelewa mpana kwa waombaji kazi kutokana na changamoto ambazo zimekua zikijitokeza kwa baadhi ya waombaji kazi kutozingatia masharti ya ujazaji wa taarifa hizo kikamilifu kwa kila kipengele kabla ya kutuma maombi ya kazi.  
Wapo baadhi ya waombaji kazi ambao wamekuwa wakijaza taarifa ambazo hazihusiani na kipengele husika hali inayoleta changamoto katika uchambuzi wa taarifa zao kwenye mfumo. Kwa kuzingatia changamoto hiyo na ili kukuza uelewa zaidi kwa waombaji kazi kupitia mfumo huo, yafuatayo ni maelezo muhimu yanayotakiwa kujazwa kwa kila kipengele kilichopo kwenye mfumo.

Tuesday, November 24, 2015

Pic of the Day

Mshindi wa ‪#‎AirtelTRACEMusicStar‬ @Mayungaa akiwa na @AKON 
nchini Marekani ambapo ameenda kwa ajiri ya kurekodi single moja 
na Star huyo wa Ghetto.

Mitandao ya Kijamii Kenya na Rais Magufuli wa Tanzania


Uchapakazi wa Rais Dkt John Magufuli unatuma ujumbe si kwa maafisa wa Tanzania pekee, bali na nchi za jirani pia na kuwaacha viongozi wa nchi hizo kwenye wakati mgumu. Kenya ambayo imekuwa ikifuatilia siasa za Tanzania tangu wakati wa kampeni, imeonesha kupenda mbinu za Magufuli na wananchi wake wanatamani mtu kama yeye.



Kwa kipindi kifupi alichoingia madarakani, Magufuli amefanya mambo makubwa na wananchi wamependa.
Ziara yake ya kushtukiza kwenye hospitali ya Muhimbili ilifichua uovu mwingi na kupelekea kufutwa kwa bodi ya wakurugenzi wa hospitali hiyo na kumuondoa Kaimu Mkurugenzi wake, Dk Hussein Kidanto. Ili kupunguza matumizi makubwa ya fedha za serikali kwaajili ya kugharamia safari za nje za viongozi wa nchi, Magufuli aliamua kuzisitisha mara moja. Dkt Magufuli pia alielekeza kiasi cha shilingi milioni 225 zilichangwa kwaajili ya kugharamia hafla ya wabunge kupongezana mjini Dodoma 

zipelekwe kwenda kununua vitanda. Badala yake shilingi milioni 15 pekee zilitumika kwaajili ya sherehe hiyo.



Siku chache baadaye vitanda hivyo na vifaa vingine vilinunuliwa na kupelekwa Muhimbili. Jumatatu hii Magufuli alitangaza kuondoa sherehe za maadhimisho ya siku ya Uhuru 
December 9 na fedha za maandalizi hayo zitumike kwa mambo mengine muhimu. Hayo na mambo mengine yamefanya Dkt Magufuli atrend nchini Kenya. 

Hizi ni baadhi ya tweets za wakenya: 

Tuesday, September 8, 2015

Kenya yaanzisha operesheni kuzima Alshabab

Rais Kenyatta amemuagiza inspekta mkuu wa polisi kuendesha operesheni dhidi ya ugaidi.


Operesheni hiyo inayoendeshwa na vikosi maalum vya kupambana na ugaidi kwa ushirikiano na jeshi la taifa linalenga wapiganaji takriban mia tatu wa Jeysh al Ayman wanaosadikika kujificha katika msitu huo. Kundi hilo la Jeysh al Ayman linasadikiwa kuwa na uhusiano na wapiganaji wa Al Shabaab

Sunday, September 6, 2015

RAMSEY NOAH: Mimi na Siasa mbalimbali


Wakati wimbi la kisiasa likiwachukua wasanii wengi wa Tanzania kutoka tasnia ya muziki na wale wa maigizo( Bongo Movie), nchini Nigeria imekuwa tofauti kwa msanii wa maigizo nchini humo Ramsey Noah, ambaye pia ni staa wa movie ya Kibongo The Devil Kingdom aliyoshirikishwa na Marehemu Stevene Kanumba. Akizungumza na mtandao wa NET Nouah amekaririwa akisema kuwa

RAMSEYNOAHINTERVIEW
yuko tofauti kabisa na wasanii wenzake wa nchini humo wanaokimbilia kwenye siasa kila kukicha na kuongeza kuwa mashabiki wake wasitegemee Ramsey kujiunga na siasa.
Akifanyiwa mahojiano maalum na mtandao wa NET wa nchini humo, Ramsey alisema kuwa: ‘Sijui jinsi gani naweza kuwa mwanasiasa, mimi sio mwanadiplomasia kivile. Sijui namna ya kuyapangilia maneno yakafana kama wanasiasa wanavyoweza kufanya. Mimi siko hivyo’.
Source: NaijaGists.com

ACACIA Yaidhamini Stendi United kwa Kitita cha shilingi bilioni moja


Kampuni ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ya Acacia iliingia mkataba wa miaka miwili na timu ya Stend United ya Mkoani Shinyanga kwa ajili ya kushiriki ligi kuu ya Vodacom ambayo inategemewa kuanza tutimua vumbi katikati ya mwezi huu. Stand United ni moja kati ya timu bora kabisa katika kanda ya ziwa ambayo imeshiriki katika ligi kuu msimu uliopita 2014/2015 na kumaliza ikiwa nafasi ya tisa.
 

Mwenyekiti wa stand united Amani Vicent (kushoto) akibadilishana mkataba wa udhamini wa timu hiyo na Makamu wa rais wa ACACIA anaeshugulikia masuala ya Kampuni, Deo Mwanyika mara baada ya kutiliana saini mkataba wa miaka miwili na kampuni hiyo.

Al Shabab wateka miji miwili kusini mwa Somalia

 http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/fec01bb37336bdc554b56465a0fd13d5_XL.jpg
Magaidi wa kundi la al Shabab wamedai kuchukua udhibiti wa miji miwili kusini magharibi mwa Somalia siku chache tu baada ya kushambulia kituo cha vikosi vya Umoja wa Afrika katika eneo hilo.
Msemaji wa al Shabab amesema kundi hilo limeteka miji miwili midogo katika eneo la Lower Shabelle ambayo ni El Saliindi, yapata kilomita 65 kusini mwa Mogadishu na Kuntuwarey katika barabara ya Mogadishiu-Barawe.