Kiungo mshambuliaji wa klabu ya real Madrid ya
nchini Hispania Gareth Bale amekiri kuwa ilikuwa ni njozi yake kuisaidia klabu yake kutwaa taji la kombe la ulaya( UEFA) baada ya
kushinda ushindi wa magoli 4-1 dhidi ya klabu ya Atletico Madrid katika muda wa
nyongeza.
Akiongea na
Skysports baada ya mchezo huo wa fainali, mchezaji huyo raia wa Wales
aliyesajiliwa na real madrid msimu
uliopita akitokea klabu ya Tottenham ya nchini uingereza aliipatia goli la pili
Madrid katika dakika ya 110 kwa mpira wa kichwa.
“Hiki ndicho
mchezaji yeyote wa mpira wa miguu huota, kushinda taji la klabu bingwa ulaya,
hakuna kitu kingine kikubwa katika ngazi ya kilabu kama taji hili.’’
“Ni hisia na furaha
isiyoelezeka na itakuwa ni kumbukumbu milele. Kitu kikubwa kwangu ni kuwa
tumecheza kama timu usiku wa leo na kutwaa taji ambalo ni la 10 kwa real Madrid.
Nimekuja Madrid kwa
pesa, nimekuja kucheza katika mashindano makubwa na kushinda mataji kama
tulivyofanya msimu huu.
Bale ambaye alikosa
nafasi kadhaa kabla ya kuwafungia mabingwa hao goli muhimu ametoa pongenzi kwa Atletico
Madrid ambao walinyakua ubingwa wa ligi ya Hispania mbele ya FC Barcelona na
Real Madrid.
Aidha. katika mchezo
huo beki wa kushoto wa timu ya taifa ya Brazil Marcelo ndiye aliyeipatia Madrid
bao la tatu kabla ya Cristiano Ronaldo kukamilisha ushindi huo kwa goli la nne
alilolifunga kwa penalty na hivyo kuibuka mfungaji bora wa mashindano hayo kwa
kuweka rekodi ya kufunga jumla ya magoli 17.
0 comments:
Post a Comment