Wabunge
wa Kenya wametofautiana vikali bunge na kuvuana mashati huku
wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswaada tatanishi wa usalama
ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge
lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili
mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao
maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye
utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani wlaipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
Seneta Johnston Muthama alijikuta pabaya kwani suruali yake iliraruliwa katika mvutano bungeni humo
Mwenyekiti wa kamati ya usalama
wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko
yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na
kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.
Spika
wa bunge Justin Muturi wakati mmoja alimuru walinzi wa bunge kuwaondoa
baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa
kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao
umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi
nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa
kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.
Seneta Muthama pia alijeruhiwa vibaya mguuni
Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.
Pia
ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa
faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha
ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.
Mswada huu umetolewa
kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab
wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia.
Rais
Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui
mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari
la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Chama cha
vilabu vikubwa vya soka barani ulaya (ECA) wanataka michuano ya kombe
la dunia ya mwaka 2022 yatayofanyika nchi Qatar yafanyike kati ya Mei 5
na Juni 4.
Shirikisho
la soka duniani Fifa walitangaza mwezi uliopita kuwa michezo ya
michuano hiyo itafanyika kati ya Januari na Februari au Novemba na
desemba. Lakini
mapendekezo yanayotolewa na Chama cha vilabu vikubwa vya soka (ECA) na
wakilishi wa ligi za kulipwa ulaya (EPFL) wanataka mashindano hayo
yacheze mwanzo mwa majira ya joto sababu itakua ndio salama kwa afya za
wachezaji.
Uamuzi wa shirikisho la mpira dunia Fifa kuhusu wakati gani michuano hiyo ifanyike inatarajiwa kutolewa Machi mwaka 2015.ECA na
EPF wanaamini pendekezo yao mpya yanaonyesha jinsi mashindano inaweza
kuchezwa Mei na Juni bila kuhatarisha afya za wachezaji na viongozi.
Pia
kufanyika kwa kombe la dunia mwezi mei na juni kutakua hakuna madhara
kwa michuano ya klabu bigwa barani ulaya, michezo ya olimpiki na waumini
wa dini ya kiislam watakua wamemaliza mfungo mtukufu wa Ramadhani
Staa
wa Bongo Fleva,Diamond Platinumz amekwea pipa leo kuelekea nchini
Uganda kwenye ''''White Paty'' inayoandaliwa na anayedaiwa kuwa ni
mpenzi wake wa sasa aishiye nchini humo. Zari.Kupitia mtandao wa
Instagram Diamond aliandika hivi.....KAMPALA!!! UGANDA!!! your boy is on
his way... #Zari_AllWhite_CirocParty. Zari The boss lady.
Source: Clouds fm
Bila
shaka kila aliekua anawafatilia au kusikia taarifa za hawa watoto
atakua na hamu ya kujua kimeendelea nini baada ya kupelekwa kutibiwa
nchini India ambapo mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete amethibitisha
kupitia ukurasa wake wa twitter kwa kuyaandika haya.
‘Hospitali ya Apollo lndia imefanikiwa kuwatenganisha watoto mapacha toka Tanzania waliokuwa wameungana vifua‘ Source: Millard Ayo
CHAMA Cha
Mapinduzi (CCM) kimevipongeza vyama vingine vya siasa nchini kwa
ushiriki wao kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwataka waongeze
kasi kwani ushindi wao wa asilimia 14 hadi sasa ni mdogo, ukilinganisha
na umri wa mfumo wa vyama vingi nchini ambao ni miaka 20.
Akizungumza
jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri
Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Nape Nnauye alisema vyama vya upinzani
vinapaswa kupongezwa kwa kushiriki kwenye uchaguzi huo na kwamba kwa
maeneo waliyoshinda wanapaswa kuwaletea maendeleo wananchi, ili
wasipoteze imani kwao.
Alisema
pamoja na ushindi huo, vyama hivyo visitarajie mabadiliko makubwa kwenye
uchaguzi mkuu wa mwakani wa madiwani, wabunge na Rais, kwani pamoja na
kupata asilimia hizo 14, hali haitabadilika ukilinganisha na ushindi wa
CCM.
“Ni kweli
pamoja na kwamba uchaguzi kama huu uliopita CCM ilishinda kwa asilimia
96 na mwaka huu kwa asilimia 84, bado sio kigezo cha vyama vya upinzani
kufanya vizuri zaidi ya asilimia hizo 14 walizoambulia hadi sasa kwa
maeneo ambayo matokeo yametoka”, alisema Nape.
Alisema
hata maeneo ambayo uchaguzi utarudiwa, sio rahisi vyama hivyo kupata
ushindi wa kishindo, kwani hadi sasa wameshaona mwelekeo wa kukubalika
kwao kwa wananchi.
Alisema
kwa matokeo hayo, vyama vya upinzani zinapaswa kuongeza kasi kwani tangu
mfumo wa vyama vingi uanze kutumika nchini ni miaka 20 sasa na bado
vyama hivyo havijakua ipasavyo.
Transparency International yasema rushwa ni tatizo kwa wote
Riport na DW
Katika ripoti yake ya leo (03.12.2014) shirika hilo lilisema rushwa
inaonekana kukithiri Uturuki na China na limetaka kuwepo ushirikiano wa
karibu wa kimataifa kuangamiza kabisa rushwa na matumizi mabaya ya
madaraka.
Katika ripoti yake shirika la Transparency International hilo lenye
makao yake Berlin Ujerumani lilisema rushwa ni tatizo kwa uchumi na kuna
umuhimu wa taasisi kubwa za fedha katika Umoja wa Ulaya na Marekani
kufanya kazi pamoja na nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi kuwakomesha
mafisadi wasikwepe mkono wa sheria.
Katika faharasa ya 20 inayoonyesha viwango vya rushwa katika mataifa
175, China imepata alama 36 kati ya 100, Uturuki imepata 45 na Angola
19, zikiwa nchi ambazo zimeanguka kwa alama kati ya 4 na 5, licha ya
uchumi wao kukua kwa wastani wa asilimia 4 katika kipindi cha miaka
minne iliyopita. Transparency International hutoa alama 100 kwa nchi
ambayo haina visa vya rushwa na sufuri kwa nchi ambayo rushwa
imeshamiri.
Kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki, Rwanda imefanya vyema katika
kupambana na rushwa ikishikilia nafasi ya 55, ikifuatiwa na Tanzania
katika nafasi ya 119, na Uganda ni ya tatu katika nafasi ya 142. Kenya
ni ya nne katika nafasi ya 145 na Burundi inashika mkia katika jumuiya
ya Afrika Mashariki ikiwa katika nafasi ya 159.
Zaidi ya theluthi mbili kati ya nchi 175 katika faharasa hiyo
zimepata pointi chini ya 50 huku Somalia, Korea Kaskazini, Sudan,
Afghansitan na Sudan Kusini kwa mara nyingine tena zikishika nafasi za
chini.
Mkurugenzi wa Transparency International katika mataifa yaliyo kusini
mwa jangwa la Sahara, Chantal Uwimana, alisema, "Vipindi vya mizozo
huchochea rushwa, kuyumba kwa hali ya kisiasa na kukosekana uthabiti kwa
sababu mifumo hudhoofika au wale wanaotakiwa kuisimamia mifumo hii
wanapoteza muelekeo.Si jambo la kushangaza kwamba Sudan Kusini na
Somalia ambazo zimekabiliwa na vita kwa muda mrefu zinaonekana kuwa na
vitendo vya rushwa iliyokithiri."
Denmark ni mfano wa kuigwa
Nchi iliyofanya vizuri kabisa na kushika nafasfi ya kwanza ni Denmark
ikijipatia pointi 92, ikifuatiwa na New Zealand, Finland, Sweden na
Norway, zote kwa mara nyingine tena zikiwa katika tabaka la nchi tano za
kwanza aktika faharasa ya rushwa.
Faharasa kuhusu rushwa ya mwaka 2014
Ukraine ilipata pointi 26 na kubakia kuwa nchi inayoongoza kwa
kiwango kikubwa cha rushwa barani Ulaya. Italia,Ugiriki na Romania kwa
pamoja zimafanya vibaya miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya
zikiwa na pointi 43.
Mwenyekiti wa Transparency International, José Ugaz alisema maafisa
mafisadi huficha mali walizozipata kwa njia isiyo halali na kuzificha
katika maeneo salama kupitia kampuni. Ugaz aidha amesema ufisadi mkubwa
katika nchi zenye uchumi mkubwa haukandamizi tu haki za binadamu kwa
watu masikini, bali pia husababisha matatizo ya utawala na uthabiti.
Ripoti hiyo ilizitaka nchi zinazoshika mkia katika orodha
iliyochapishwa zichukue hatua madhubuti za makusudi kupambana na rushwa
kwa masilahi ya umma. Ugaz aliyataka mataifa yanayoshika nafasi za juu
katika faharasa hiyo yasieneze vitendo vya ufisadi katika nchi ambazo
hazijaendelea.
Shirika la Transparency International liliuhimiza Umoja wa Ulaya,
Marekani na kundi la G20 la mataifa yaliyostawi na yanayoinukia
kiuchumi, kuiga mfano wa Denmark na kuanzisha daftari la umma
linalojumuisha tarifa muhimu za wamiliki kwa kampuni zote
zilizoshirikishwa.
AKA ni miongoni mwa rappers wakali Africa ambaye hivi karibuni
alikuwa South Africa na alishinda tuzo moja ya Channel O ambako pia
Diamond alikuwepo huko. Aka ame Repost video ya mapokezi ya Diamond
iliyowekwa Sammisago.com na Kwenye Instagram ya Sammisago huku akiweka huu ujumbe.
“Diamond
lands back in Tanzania after winning 3 Channel O Awards and this
happens … Imagine South Africans felt like this about their own artists …
In my country this is something reserved for the Bieber’s and Breezy’s …
Where is our pride? Where is our passion? Anyways … BIG UP DIAMOND. ”