Thursday, December 18, 2014

Wabunge warushiana ngumi bungeni Kenya


Wabunge wa Kenya wametofautiana vikali bunge na kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswaada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.

Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani wlaipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
 
 Seneta Johnston Muthama alijikuta pabaya kwani suruali yake iliraruliwa katika mvutano bungeni humo

Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.

Spika wa bunge Justin Muturi wakati mmoja alimuru walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.

Mswada huo ambao umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.


 
Seneta Muthama pia alijeruhiwa vibaya mguuni

Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.

Pia ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.

Mswada huu umetolewa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia.

Rais Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Source: BBC

Kombe la Dunia kuchezwa Mei na June?




Chama cha vilabu vikubwa vya soka barani ulaya (ECA) wanataka michuano ya kombe la dunia ya mwaka 2022 yatayofanyika nchi Qatar yafanyike kati ya Mei 5 na Juni 4. 
 
Shirikisho la soka duniani Fifa walitangaza mwezi uliopita kuwa michezo ya michuano hiyo itafanyika kati ya Januari na Februari au Novemba na desemba.  Lakini mapendekezo yanayotolewa na Chama cha vilabu vikubwa vya soka (ECA) na wakilishi wa ligi za kulipwa ulaya (EPFL) wanataka mashindano hayo yacheze mwanzo mwa majira ya joto sababu itakua ndio salama kwa afya za wachezaji.
 
Uamuzi wa shirikisho la mpira dunia Fifa kuhusu wakati gani michuano hiyo ifanyike inatarajiwa kutolewa Machi mwaka 2015. ECA na EPF wanaamini pendekezo yao mpya yanaonyesha jinsi mashindano inaweza kuchezwa Mei na Juni bila kuhatarisha afya za wachezaji na viongozi.

 Pia kufanyika kwa kombe la dunia mwezi mei na juni kutakua hakuna madhara kwa michuano ya klabu bigwa barani ulaya, michezo ya olimpiki na waumini wa dini ya kiislam watakua wamemaliza mfungo mtukufu wa Ramadhani 

.Source: Mjengwa

Wednesday, December 17, 2014

Diamond akwea pipa aenda Uganda kwenye ''White Paty'' ya Zari

Staa wa Bongo Fleva,Diamond Platinumz amekwea pipa leo kuelekea nchini Uganda kwenye ''''White Paty'' inayoandaliwa na anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake wa sasa aishiye nchini humo. Zari.Kupitia mtandao wa Instagram Diamond aliandika hivi.....KAMPALA!!! UGANDA!!! your boy is on his way... #Zari_AllWhite_CirocParty.
Zari The boss lady.
Source: Clouds fm

Hii taarifa inawahusu wale watoto wawili wa Tanzania waliokua wameungana vifua.



Watoto 1Bila shaka kila aliekua anawafatilia au kusikia taarifa za hawa watoto atakua na hamu ya kujua kimeendelea nini baada ya kupelekwa kutibiwa nchini India ambapo mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete amethibitisha kupitia ukurasa wake wa twitter kwa kuyaandika haya.
Hospitali ya Apollo lndia imefanikiwa kuwatenganisha watoto mapacha toka Tanzania waliokuwa wameungana vifua‘
Source: Millard Ayo

NAPE APONGEZA WAPINZANI

NapeNnauye_480_280_2238a.jpg

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimevipongeza vyama vingine vya siasa nchini kwa ushiriki wao kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwataka waongeze kasi kwani ushindi wao wa asilimia 14 hadi sasa ni mdogo, ukilinganisha na umri wa mfumo wa vyama vingi nchini ambao ni miaka 20.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Nape Nnauye alisema vyama vya upinzani vinapaswa kupongezwa kwa kushiriki kwenye uchaguzi huo na kwamba kwa maeneo waliyoshinda wanapaswa kuwaletea maendeleo wananchi, ili wasipoteze imani kwao.

Alisema pamoja na ushindi huo, vyama hivyo visitarajie mabadiliko makubwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwakani wa madiwani, wabunge na Rais, kwani pamoja na kupata asilimia hizo 14, hali haitabadilika ukilinganisha na ushindi wa CCM.

“Ni kweli pamoja na kwamba uchaguzi kama huu uliopita CCM ilishinda kwa asilimia 96 na mwaka huu kwa asilimia 84, bado sio kigezo cha vyama vya upinzani kufanya vizuri zaidi ya asilimia hizo 14 walizoambulia hadi sasa kwa maeneo ambayo matokeo yametoka”, alisema Nape.

Alisema hata maeneo ambayo uchaguzi utarudiwa, sio rahisi vyama hivyo kupata ushindi wa kishindo, kwani hadi sasa wameshaona mwelekeo wa kukubalika kwao kwa wananchi.
Alisema kwa matokeo hayo, vyama vya upinzani zinapaswa kuongeza kasi kwani tangu mfumo wa vyama vingi uanze kutumika nchini ni miaka 20 sasa na bado vyama hivyo havijakua ipasavyo. 
Source: Mjengwa blog

Wednesday, December 3, 2014

RUSHWA SI AFRIKA PEKEE , NI UGONJWA UNAOSUMBUA SASA HATA NCHI ZILIZOENDELEA

Transparency International yasema rushwa ni tatizo kwa wote

Riport na DW

Katika ripoti yake ya leo (03.12.2014) shirika hilo lilisema rushwa inaonekana kukithiri Uturuki na China na limetaka kuwepo ushirikiano wa karibu wa kimataifa kuangamiza kabisa rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.
Katika ripoti yake shirika la Transparency International hilo lenye makao yake Berlin Ujerumani lilisema rushwa ni tatizo kwa uchumi na kuna umuhimu wa taasisi kubwa za fedha katika Umoja wa Ulaya na Marekani kufanya kazi pamoja na nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi kuwakomesha mafisadi wasikwepe mkono wa sheria.

Katika faharasa ya 20 inayoonyesha viwango vya rushwa katika mataifa 175, China imepata alama 36 kati ya 100, Uturuki imepata 45 na Angola 19, zikiwa nchi ambazo zimeanguka kwa alama kati ya 4 na 5, licha ya uchumi wao kukua kwa wastani wa asilimia 4 katika kipindi cha miaka minne iliyopita. Transparency International hutoa alama 100 kwa nchi ambayo haina visa vya rushwa na sufuri kwa nchi ambayo rushwa imeshamiri.

Kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki, Rwanda imefanya vyema katika kupambana na rushwa ikishikilia nafasi ya 55, ikifuatiwa na Tanzania katika nafasi ya 119, na Uganda ni ya tatu katika nafasi ya 142. Kenya ni ya nne katika nafasi ya 145 na Burundi inashika mkia katika jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa katika nafasi ya 159.

Zaidi ya theluthi mbili kati ya nchi 175 katika faharasa hiyo zimepata pointi chini ya 50 huku Somalia, Korea Kaskazini, Sudan, Afghansitan na Sudan Kusini kwa mara nyingine tena zikishika nafasi za chini.

Mkurugenzi wa Transparency International katika mataifa yaliyo kusini mwa jangwa la Sahara, Chantal Uwimana, alisema, "Vipindi vya mizozo huchochea rushwa, kuyumba kwa hali ya kisiasa na kukosekana uthabiti kwa sababu mifumo hudhoofika au wale wanaotakiwa kuisimamia mifumo hii wanapoteza muelekeo.Si jambo la kushangaza kwamba Sudan Kusini na Somalia ambazo zimekabiliwa na vita kwa muda mrefu zinaonekana kuwa na vitendo vya rushwa iliyokithiri."

Denmark ni mfano wa kuigwa

 Nchi iliyofanya vizuri kabisa na kushika nafasfi ya kwanza ni Denmark ikijipatia pointi 92, ikifuatiwa na New Zealand, Finland, Sweden na Norway, zote kwa mara nyingine tena zikiwa katika tabaka la nchi tano za kwanza aktika faharasa ya rushwa.
Infografik Korruptionsindex 2014 Englisch  
Faharasa kuhusu rushwa ya mwaka 2014

Ukraine ilipata pointi 26 na kubakia kuwa nchi inayoongoza kwa kiwango kikubwa cha rushwa barani Ulaya. Italia,Ugiriki na Romania kwa pamoja zimafanya vibaya miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zikiwa na pointi 43.

Mwenyekiti wa Transparency International, José Ugaz alisema maafisa mafisadi huficha mali walizozipata kwa njia isiyo halali na kuzificha katika maeneo salama kupitia kampuni. Ugaz aidha amesema ufisadi mkubwa katika nchi zenye uchumi mkubwa haukandamizi tu haki za binadamu kwa watu masikini, bali pia husababisha matatizo ya utawala na uthabiti.

Ripoti hiyo ilizitaka nchi zinazoshika mkia katika orodha iliyochapishwa zichukue hatua madhubuti za makusudi kupambana na rushwa kwa masilahi ya umma. Ugaz aliyataka mataifa yanayoshika nafasi za juu katika faharasa hiyo yasieneze vitendo vya ufisadi katika nchi ambazo hazijaendelea.
Shirika la Transparency International liliuhimiza Umoja wa Ulaya, Marekani na kundi la G20 la mataifa yaliyostawi na yanayoinukia kiuchumi, kuiga mfano wa Denmark na kuanzisha daftari la umma linalojumuisha tarifa muhimu za wamiliki kwa kampuni zote zilizoshirikishwa.

HUYU DIAMOND PLATNAMZ TAYARI AMEISHIKA AFRIKA HIVI HIVI KIUTANI UTANI


Post Ya Msanii AKA Kuhusu Mapokezi Ya Diamond Tanzania.

By 
Aka
AKA ni miongoni  mwa rappers wakali Africa ambaye hivi karibuni alikuwa South Africa na alishinda tuzo moja ya Channel O  ambako pia Diamond alikuwepo huko. Aka ame Repost video ya mapokezi ya Diamond iliyowekwa Sammisago.com na Kwenye Instagram ya Sammisago huku akiweka huu ujumbe.
Diamond lands back in Tanzania after winning 3 Channel O Awards and this happens … Imagine South Africans felt like this about their own artists … In my country this is something reserved for the Bieber’s and Breezy’s … Where is our pride? Where is our passion? Anyways … BIG UP DIAMOND.
aka 2 Aka