CHAMA Cha
Mapinduzi (CCM) kimevipongeza vyama vingine vya siasa nchini kwa
ushiriki wao kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwataka waongeze
kasi kwani ushindi wao wa asilimia 14 hadi sasa ni mdogo, ukilinganisha
na umri wa mfumo wa vyama vingi nchini ambao ni miaka 20.
Akizungumza
jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri
Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Nape Nnauye alisema vyama vya upinzani
vinapaswa kupongezwa kwa kushiriki kwenye uchaguzi huo na kwamba kwa
maeneo waliyoshinda wanapaswa kuwaletea maendeleo wananchi, ili
wasipoteze imani kwao.
Alisema
pamoja na ushindi huo, vyama hivyo visitarajie mabadiliko makubwa kwenye
uchaguzi mkuu wa mwakani wa madiwani, wabunge na Rais, kwani pamoja na
kupata asilimia hizo 14, hali haitabadilika ukilinganisha na ushindi wa
CCM.
“Ni kweli
pamoja na kwamba uchaguzi kama huu uliopita CCM ilishinda kwa asilimia
96 na mwaka huu kwa asilimia 84, bado sio kigezo cha vyama vya upinzani
kufanya vizuri zaidi ya asilimia hizo 14 walizoambulia hadi sasa kwa
maeneo ambayo matokeo yametoka”, alisema Nape.
Alisema
hata maeneo ambayo uchaguzi utarudiwa, sio rahisi vyama hivyo kupata
ushindi wa kishindo, kwani hadi sasa wameshaona mwelekeo wa kukubalika
kwao kwa wananchi.
Alisema
kwa matokeo hayo, vyama vya upinzani zinapaswa kuongeza kasi kwani tangu
mfumo wa vyama vingi uanze kutumika nchini ni miaka 20 sasa na bado
vyama hivyo havijakua ipasavyo.
Source: Mjengwa blog
0 comments:
Post a Comment