Wabunge
wa Kenya wametofautiana vikali bunge na kuvuana mashati huku
wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswaada tatanishi wa usalama
ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.
Bunge
lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili
mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao
maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye
utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani wlaipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
Seneta Johnston Muthama alijikuta pabaya kwani suruali yake iliraruliwa katika mvutano bungeni humo
Mwenyekiti wa kamati ya usalama
wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko
yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na
kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.
Spika
wa bunge Justin Muturi wakati mmoja alimuru walinzi wa bunge kuwaondoa
baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa
kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.
Mswada huo ambao
umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi
nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa
kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.
Seneta Muthama pia alijeruhiwa vibaya mguuni
Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.
Pia
ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa
faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha
ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.
Mswada huu umetolewa
kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab
wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia.
Rais
Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui
mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari
la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Bill Cosby atakiwa mahakani
Image copyrightREUTERS
Jaji nchini Marekani ameamuaru mchekeshaji, Bill Cosby, kusimama mahakamani dhidi ya kesi kwa madai ya unyanyasaji wa kijinsia.
Cosby anatuhumiwa kwa makosa ya kumdhalilisha wanawake katika makazi…Read More
Aliyesababisha Mandela akamatwe akiri
Image copyrightBImage captionMandela alikamatwa mwaka 1962 saa za usiku karibu na mji wa Durban.
Ajenti mmoja wa zamani wa shirika la ujasusi la marekani CIA, amekiri kuwa ndiye aliwafahamisha polisi wa Afrika kusini a…Read More
Upasuaji kwa njia ya Roboti
Hospitali moja katika manispaa ya Chongqing nchini China imefaulu kutumia roboti kufanya upasuaji wa kutoa uvimbe kutoka mwili wa mgonjwa wa saratani ya kongosho.Hospitali hiyo imesema kuwa huo ulikuwa upasuaj…Read More
Hii ndiyo Meli Mpya Kubwa Duniani, Inachukua Abiria 6,780
Mapema wiki hii meli ambayo ina uwezo wa kuchukua abiria 6,780 iling’oa nanga Southampton kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kabla ya uzinduzi rasmi, Watu 3000 wamepata bahati kupanda meli hii kubwa duniani. Mel…Read More
0 comments:
Post a Comment