
“Mimi Nijiuzulu kwa sababu gani? yaani kwa sababu ya mafanikio ya kuwakomboa wanawake kwenye Elimu ndio mimi nijuzulu,maana kujiuzulu kunasababu, na hakuna sababu ya mimi kufanya hivyo na sitofanya hivyo kwani wanaodai mimi nijiuzulu ni wanafiki wenye nia mbaya na mimi ,na mimi sijiuzulu ng’o na nikifanya wanavyotaka Rais atashangaa ”alisema Waziri Tibaijuka.
“Leo natuhumiwa na kila mtu kwamba nimepewa pesa na Rugimalira kwamba ni za kifisadi,Jamani tuwe wa kweli kuhusu madai haya maana nimepewa pesa na Rugemalira kwa ajiri ya shule hizi na sio huyo pekee alliyechangia kwani waliochangia pesa hizi ni watu wengi ikiwema Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, Mfanya Biashara Maarufu Reginald Mengi na wengine wengi,inakuwaje leo mchango wa Rugumarila kwa Ajiri ya Elimu kwenye Shule hii ndio iwe nongwa”
“Kwasababu ukisema ni pesa alizonipa ni za ufisadi wa Escrow sio
kweli,kwani Bodi ya Shule ilimuomba Bwana Rugemalira pesa kwa kutumia
Kampuni yake ya Mabibo Wine na kipindi kile ndio alikuwa kiongozi, sasa
hawa watu wanaozani ni za ufisadi inakuwaje jamani tuwe
wakweli”Aliongeza Waziri Tibaijuka."
Source: Clouds fm radio
Source: Clouds fm radio
0 comments:
Post a Comment