Viongozi
wa Ulaya wamemaliza kikao chao mjini Brussels Ubelgiji, wakisema kwa
sasa wameungana zaidi kuliko ilivyokuwa awali katika kuikabili Urusi. Viongozi
hao wameonesha kuwa vikwazo vya kiuchumi havitadhoofishwa licha ya
matatizo ya kifedha yanayoikabili Urusi.
Badala yake hatua mpya za Umoja wa Ulaya zilizokuwa zimewekwa kufuatia Urusi kulitwaa kimabavu jimbo la Crimea zimepitishwa na zitaanza kutumika mwishoni mwa wiki hii.
Rais
mpya wa Baraza la Ulaya, Donald Tusk akifunga kikao cha viongozi wa EU
amesema Urusi na vitendo vyake ni tatizo kubwa la kimkakati
linaloikabili Ulaya.
Akiongoza kikao cha wakuu wa nch ishirini na nane za Umoja wa Ulaya. Bw. Tusk amesema kuwa vitendo vya Urusi ndani ya Ukraine na katika Ulaya ni changamoto na alibaini kwamba mataifa ya Umoja wa Ulaya yameungana zaidi kuliko ilivyowahi kuwa huko nyuma katika kukabiliana na Urusi.
Aidha, ameonya kuwa Ulaya inahitaji mkakati wa muda mrefu wa
aina yake,ambao si tu utakaoshughulikia matatizo katika wiki zijazo na
miezi, bali miaka. Wakati huo huo viongozi wamekubaliana vikwazo vipya
vinavyopiga marufuku uwekezaji katika jimbo la Crimea, ishara kwamba
vikwazo hivyo havitalegezwa hadi Urusi itakapobadili msimamo wake kuhusu
jimbo hilo.
Source: BBC
0 comments:
Post a Comment