Friday, December 19, 2014

Video Ya AliKiba Kutoka Leo, Itarushwa Kwenye Vituo Hivi Kwa Mara Ya Kwanza

Video iliyosubiriwa kwa muda mrefu na mashabiki wa Ali Kiba ‘Mwana’itaanza kuonyeshwa ijumaa ya leo December 19 2014. Ali Kiba amethibitisha kuwa video imekamilika kwa kutoa kionjo cha video hio na kusema ‘Video imetayarishwa na muongozaji kutoka Afrika Kusini na imefanyika maeneo ya mjii wa Cape Town” .

Vituo vitakavyo rusha hii video

Cameroon, Ethiopia, Angola, U.S. & U.K. itachezwa kwenye vituo vya 1Musicnetworks.

Nigeria na Ghana itachezwa kwenye kituo cha SOUNDCITYtv.

Uganda itachezwa kwenye kituo cha NTV Uganda.

Kenya itachezwa kwenye kituo cha Citizen Tv kwenye kipindi cha Mseto.

Tanzania itachezwa kwenye kituo cha CloudsTV.
SOURCE :Dj Fetty blog

Balotelli afungiwa mchezo mmoja na faini

Chama cha Soka nchini Uingereza, kimemfungia mchezo mmoja, mshambuliaji wa Liverpool, Mario Balotelli ikiwa ni adhabu kutokana na kile Super Mario alichokiandika katika mitandao ya habari ya kijamii. Adhabu hiyo itamlazimisha nyota huyo wa Italia, kukosa mchezo wakati timu yake ya Liverpool itakapoikaribisha Arsenal Jumapili, katika michezo ya ligi kuu ya England. Pia amepigwa faini ya pauni£25,000 na lazima ahudhurie kozi ya elimu.
 

Baloteli mwenye umri wa miaka 24 ameadhibiwa kwa mujibu wa sheria za FA kwa kutuma ujumbe ambao umeonekana kuwa na ubaguzi. Balotelli amekubali adhabu hiyo lakini ameiandikia FA ili iweze kumpunguzia, baada ya kujua adhabu yake, aliandika katika ukurasa wake rasmi wa Facebook kwamba uamuzi wa FA "umeonyesha wazi" kwamba ujumbe wake ulikuwa "makosa".

Balotelli aliituma picha iliyotolewa na mtu mwingine tofauti. Alisema: "nasikitika kwamba wachezaji wenzangu na mashabiki wa Liverpool FC wataadhibiwa kwa kosa ambalo nimelifanya na sasa najutia. Ni dhamira yangu kukubaliana na uamuzi wa FA na kuhakikisha kuwa halitatokea tena."
Msemaji wa Liverpool amesema: "klabu inatambua uamuzi uliofikiwa na jopo huru la FA na utapewa uzito unaostahili mara tutakapoupokea kutoka FA.

"Hatua yoyote itakayochukuliwa nasi kuhusiana na jambo hili itakuwa kati ya klabu na mchezaji."
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester City Balotelli alirudia kutuma picha ya mchezo wa kompyuta yenye kibonzo cha Super Mario katika mtandao wa Instagram ambacho kilikuwa na maneno "ruka kama mtu mweusi na kusanya sarafu kama myahudi."
Baadaye alituma ujumbe wa tweeter akikanusha kuwa ujumbe huo ulikuwa na makosa, kabla ya kuomba radhi.

Balotelli alirejea katika kikosi cha Liverpool kilichocheza na Manchester United katika uwanja wa Old Trafford Jumapili baada ya kukosa michezo sita kutokana na maumivu ya nyama za paja. Katika mchezo huo Liverpool iliambulia kipigo cha magoli 3-0.
Balotelli ameifungia magoli mawili timu yake katika mechi 15 alizoichezea timu ya Liverpool tangu atoke AC Milan msimu uliopita wa kiangazi.
Source: BBC Swahili

Jumuiya ya Ulaya yaungana dhidi ya Russia



Viongozi wa Ulaya wamemaliza kikao chao mjini Brussels Ubelgiji, wakisema kwa sasa wameungana zaidi kuliko ilivyokuwa awali katika kuikabili Urusi. Viongozi hao wameonesha kuwa vikwazo vya kiuchumi havitadhoofishwa licha ya matatizo ya kifedha yanayoikabili Urusi.

Badala yake hatua mpya za Umoja wa Ulaya zilizokuwa zimewekwa kufuatia Urusi kulitwaa kimabavu jimbo la Crimea zimepitishwa na zitaanza kutumika mwishoni mwa wiki hii.

Rais mpya wa Baraza la Ulaya, Donald Tusk akifunga kikao cha viongozi wa EU amesema Urusi na vitendo vyake ni tatizo kubwa la kimkakati linaloikabili Ulaya.

Akiongoza kikao cha wakuu wa nch ishirini na nane za Umoja wa Ulaya. Bw. Tusk amesema kuwa vitendo vya Urusi ndani ya Ukraine na katika Ulaya ni changamoto na alibaini kwamba mataifa ya Umoja wa Ulaya yameungana zaidi kuliko ilivyowahi kuwa huko nyuma katika kukabiliana na Urusi.

Aidha, ameonya kuwa Ulaya inahitaji mkakati wa muda mrefu wa aina yake,ambao si tu utakaoshughulikia matatizo katika wiki zijazo na miezi, bali miaka. Wakati huo huo viongozi wamekubaliana vikwazo vipya vinavyopiga marufuku uwekezaji katika jimbo la Crimea, ishara kwamba vikwazo hivyo havitalegezwa hadi Urusi itakapobadili msimamo wake kuhusu jimbo hilo.
Source: BBC

Thursday, December 18, 2014

MANENO YA MAMA TIBAIJUKA KATIKA MKUTANO WAKE NA WAANDISHI WA HABARI JUU YA ESCROW.



 “Mimi Nijiuzulu kwa sababu gani? yaani kwa sababu ya mafanikio ya kuwakomboa wanawake kwenye Elimu ndio mimi nijuzulu,maana kujiuzulu kunasababu, na hakuna sababu ya mimi kufanya hivyo na sitofanya hivyo kwani wanaodai mimi nijiuzulu ni wanafiki wenye nia mbaya na mimi ,na mimi sijiuzulu ng’o na nikifanya wanavyotaka Rais atashangaa ”alisema Waziri Tibaijuka.

“Leo natuhumiwa na kila mtu kwamba nimepewa pesa na Rugimalira kwamba ni za kifisadi,Jamani tuwe wa kweli kuhusu madai haya maana nimepewa pesa na Rugemalira kwa ajiri ya shule hizi na sio huyo pekee alliyechangia kwani waliochangia pesa hizi ni watu wengi ikiwema Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, Mfanya Biashara Maarufu Reginald Mengi na wengine wengi,inakuwaje leo mchango wa Rugumarila kwa Ajiri ya Elimu kwenye Shule hii ndio iwe nongwa”

“Kwasababu ukisema ni pesa alizonipa ni za ufisadi wa Escrow sio kweli,kwani Bodi ya Shule ilimuomba Bwana Rugemalira pesa kwa kutumia Kampuni yake ya Mabibo Wine na kipindi kile ndio alikuwa kiongozi, sasa hawa watu wanaozani ni za ufisadi inakuwaje jamani tuwe wakweli”Aliongeza Waziri Tibaijuka."
Source: Clouds fm radio

Rihanna aajiriwa na Puma


Msanii wa muziki nchini Marekani Rihanna anajiandaa kuanza kufanya kazi katika kampuni ya michezo Puma.Mwanamziki huyo ametangazwa kuwa mkurugenzi wa ubunifu wa vifaa vya kike na atakuwa uso wa vifaa vya mazoezi vya wanawake.
Rihana mwenye umri wa miaka 26 ataunda aina ya nguo zilizopo pamoja na viatu na kusaidia kubuni muundo mpya wa chapa cha bidhaa hizo.
Akizungumza kuhusu ushirikiano huo,Rihana amesema anafurahi kuona ni nini yeye na Puma wanaweza kubuni.

Wakuu wa kampuni ya Puma wanasema kuwa Rihana ataleta ubunifu katika ulimwengu wa riadha.
Nguo hizo mpya zitakuwa na mtindo wenye lengo la kuwaimarisha wanawake katika mazoezi mbali na kuwafanya kuamini miili yao pamoja na wao wenyewe. Jukumu la Rihana litakuwa kuwa na ushawishi katika bidhaa zitakazoundwa pamoja na kuandaa ukuzaji wa bidhaa mpya. Akiwa miongoni mwa kampeni ya Forever faster msanii huyo atashirikishwa na wanariadha kama viule Usain Bolt na Sergio Aguero.

 
Mkurugenzi wa kampuni hiyo Bjorn Gulden amesema kuwa waliamua kumtafuta mshirika katika nguo za wanawake za kufanyia mazoezi kutokana na ushawishi mkubwa wa kampuni hiyo katika soka,riadha na mashindano ya magari.Tunafurahi kumpata Rihana na tunajianda kuona ni nini tunaweza buni kwa ushirikiano wake.

Rihana si mtu wa kwanza nje ya michezo kujiunga na kampuni ya Puma. Msanii 50 cent na Jay Z walitoa viatu na kampuni ya Reebok, huku Kim Kardashian akiwa uso wa viatu vya Sketchers na mumewe Kanye West akifanya kazi na Nike pamoja na Adidas.

Wabunge warushiana ngumi bungeni Kenya


Wabunge wa Kenya wametofautiana vikali bunge na kuvuana mashati huku wakirushiana ngumi kufuatia mjadala kuhusu mswaada tatanishi wa usalama ambao wabunge wa upinzani wanasema unakiuka uhuru wa wakenya.

Bunge lililazimika kuahirisha vikao vyake kwa dakika 30 badala ya kujadili mswada tatanishi kuhusu usalama wa nchi. Kikao cha leo kilikuwa kikao maalum ambacho kilipaswa kupitisha mswada huo ambao baadaye utaidhinishwa na Rais kuwa sheria.
Wabunge wa upinzani wlaipinga mswada huo na kuanza kurusha karatasi sakafuni huku wakitatiza shughuli bungeni humo.
 
 Seneta Johnston Muthama alijikuta pabaya kwani suruali yake iliraruliwa katika mvutano bungeni humo

Mwenyekiti wa kamati ya usalama wa bunge, Bwana Asman Kamama, alijaribu kuyaja mabadiliko yaliyopendekezwa kufanyiwa mswada huo lakini wabunge walianza kuimba na kumzomea spika wa bunge wakiukataa mswada huo wakisema 'bado mapambano.

Spika wa bunge Justin Muturi wakati mmoja alimuru walinzi wa bunge kuwaondoa baadhi ya viongozi waliofika bungeni humo kwa mjhadala ambao ulitarajiwa kuwa kaa moto, hasa kw aupande wa upinzani.

Mswada huo ambao umewasilishwa bunge kufuatia matukio ya utovu wa usalama na mashambulizi nchini Kenya, unapendekeza kuwa washukiwaw augaidi wanaweza kuzuiliwa kwa mwaka mmoja huku polisi wakifanya uchunguzi.


 
Seneta Muthama pia alijeruhiwa vibaya mguuni

Mapendekezo ya mswada huo ni kwamba mshukiwa wa ugaidi anaweza kuzuiliwa kwa siku 360 kutoka siku 90 za awali.

Pia ikiwa mswada huo utapistihwa kuwa sheria, mashirika ya habari yatatozwa faini ya hadili shilingi milioni 5 kwa kuchapisha taarifa au picha ambazo zinaleta hofu na kusababisha taharuki.

Mswada huu umetolewa kufuatia mashambulizi yaliyofanywa na wapiganaji wa Al Shabaab wakilalamika na kutaka wanajeshi wa Kenya kuondolewa Somalia.

Rais Kenyatta amekuwa akikabiliwa na shinikzo kuimarisha usalama wa tangui mashambulizi ya Septemba mwaka 2013 katika jengo la maduka ya kifahari la Westgate mjini Nairobi ambapo watu 67 waliuawa.
Source: BBC

Kombe la Dunia kuchezwa Mei na June?




Chama cha vilabu vikubwa vya soka barani ulaya (ECA) wanataka michuano ya kombe la dunia ya mwaka 2022 yatayofanyika nchi Qatar yafanyike kati ya Mei 5 na Juni 4. 
 
Shirikisho la soka duniani Fifa walitangaza mwezi uliopita kuwa michezo ya michuano hiyo itafanyika kati ya Januari na Februari au Novemba na desemba.  Lakini mapendekezo yanayotolewa na Chama cha vilabu vikubwa vya soka (ECA) na wakilishi wa ligi za kulipwa ulaya (EPFL) wanataka mashindano hayo yacheze mwanzo mwa majira ya joto sababu itakua ndio salama kwa afya za wachezaji.
 
Uamuzi wa shirikisho la mpira dunia Fifa kuhusu wakati gani michuano hiyo ifanyike inatarajiwa kutolewa Machi mwaka 2015. ECA na EPF wanaamini pendekezo yao mpya yanaonyesha jinsi mashindano inaweza kuchezwa Mei na Juni bila kuhatarisha afya za wachezaji na viongozi.

 Pia kufanyika kwa kombe la dunia mwezi mei na juni kutakua hakuna madhara kwa michuano ya klabu bigwa barani ulaya, michezo ya olimpiki na waumini wa dini ya kiislam watakua wamemaliza mfungo mtukufu wa Ramadhani 

.Source: Mjengwa

Wednesday, December 17, 2014

Diamond akwea pipa aenda Uganda kwenye ''White Paty'' ya Zari

Staa wa Bongo Fleva,Diamond Platinumz amekwea pipa leo kuelekea nchini Uganda kwenye ''''White Paty'' inayoandaliwa na anayedaiwa kuwa ni mpenzi wake wa sasa aishiye nchini humo. Zari.Kupitia mtandao wa Instagram Diamond aliandika hivi.....KAMPALA!!! UGANDA!!! your boy is on his way... #Zari_AllWhite_CirocParty.
Zari The boss lady.
Source: Clouds fm

Hii taarifa inawahusu wale watoto wawili wa Tanzania waliokua wameungana vifua.



Watoto 1Bila shaka kila aliekua anawafatilia au kusikia taarifa za hawa watoto atakua na hamu ya kujua kimeendelea nini baada ya kupelekwa kutibiwa nchini India ambapo mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete amethibitisha kupitia ukurasa wake wa twitter kwa kuyaandika haya.
Hospitali ya Apollo lndia imefanikiwa kuwatenganisha watoto mapacha toka Tanzania waliokuwa wameungana vifua‘
Source: Millard Ayo

NAPE APONGEZA WAPINZANI

NapeNnauye_480_280_2238a.jpg

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimevipongeza vyama vingine vya siasa nchini kwa ushiriki wao kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kuwataka waongeze kasi kwani ushindi wao wa asilimia 14 hadi sasa ni mdogo, ukilinganisha na umri wa mfumo wa vyama vingi nchini ambao ni miaka 20.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Nape Nnauye alisema vyama vya upinzani vinapaswa kupongezwa kwa kushiriki kwenye uchaguzi huo na kwamba kwa maeneo waliyoshinda wanapaswa kuwaletea maendeleo wananchi, ili wasipoteze imani kwao.

Alisema pamoja na ushindi huo, vyama hivyo visitarajie mabadiliko makubwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwakani wa madiwani, wabunge na Rais, kwani pamoja na kupata asilimia hizo 14, hali haitabadilika ukilinganisha na ushindi wa CCM.

“Ni kweli pamoja na kwamba uchaguzi kama huu uliopita CCM ilishinda kwa asilimia 96 na mwaka huu kwa asilimia 84, bado sio kigezo cha vyama vya upinzani kufanya vizuri zaidi ya asilimia hizo 14 walizoambulia hadi sasa kwa maeneo ambayo matokeo yametoka”, alisema Nape.

Alisema hata maeneo ambayo uchaguzi utarudiwa, sio rahisi vyama hivyo kupata ushindi wa kishindo, kwani hadi sasa wameshaona mwelekeo wa kukubalika kwao kwa wananchi.
Alisema kwa matokeo hayo, vyama vya upinzani zinapaswa kuongeza kasi kwani tangu mfumo wa vyama vingi uanze kutumika nchini ni miaka 20 sasa na bado vyama hivyo havijakua ipasavyo. 
Source: Mjengwa blog

Wednesday, December 3, 2014

RUSHWA SI AFRIKA PEKEE , NI UGONJWA UNAOSUMBUA SASA HATA NCHI ZILIZOENDELEA

Transparency International yasema rushwa ni tatizo kwa wote

Riport na DW

Katika ripoti yake ya leo (03.12.2014) shirika hilo lilisema rushwa inaonekana kukithiri Uturuki na China na limetaka kuwepo ushirikiano wa karibu wa kimataifa kuangamiza kabisa rushwa na matumizi mabaya ya madaraka.
Katika ripoti yake shirika la Transparency International hilo lenye makao yake Berlin Ujerumani lilisema rushwa ni tatizo kwa uchumi na kuna umuhimu wa taasisi kubwa za fedha katika Umoja wa Ulaya na Marekani kufanya kazi pamoja na nchi zenye uchumi unaokua kwa kasi kuwakomesha mafisadi wasikwepe mkono wa sheria.

Katika faharasa ya 20 inayoonyesha viwango vya rushwa katika mataifa 175, China imepata alama 36 kati ya 100, Uturuki imepata 45 na Angola 19, zikiwa nchi ambazo zimeanguka kwa alama kati ya 4 na 5, licha ya uchumi wao kukua kwa wastani wa asilimia 4 katika kipindi cha miaka minne iliyopita. Transparency International hutoa alama 100 kwa nchi ambayo haina visa vya rushwa na sufuri kwa nchi ambayo rushwa imeshamiri.

Kwa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki, Rwanda imefanya vyema katika kupambana na rushwa ikishikilia nafasi ya 55, ikifuatiwa na Tanzania katika nafasi ya 119, na Uganda ni ya tatu katika nafasi ya 142. Kenya ni ya nne katika nafasi ya 145 na Burundi inashika mkia katika jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa katika nafasi ya 159.

Zaidi ya theluthi mbili kati ya nchi 175 katika faharasa hiyo zimepata pointi chini ya 50 huku Somalia, Korea Kaskazini, Sudan, Afghansitan na Sudan Kusini kwa mara nyingine tena zikishika nafasi za chini.

Mkurugenzi wa Transparency International katika mataifa yaliyo kusini mwa jangwa la Sahara, Chantal Uwimana, alisema, "Vipindi vya mizozo huchochea rushwa, kuyumba kwa hali ya kisiasa na kukosekana uthabiti kwa sababu mifumo hudhoofika au wale wanaotakiwa kuisimamia mifumo hii wanapoteza muelekeo.Si jambo la kushangaza kwamba Sudan Kusini na Somalia ambazo zimekabiliwa na vita kwa muda mrefu zinaonekana kuwa na vitendo vya rushwa iliyokithiri."

Denmark ni mfano wa kuigwa

 Nchi iliyofanya vizuri kabisa na kushika nafasfi ya kwanza ni Denmark ikijipatia pointi 92, ikifuatiwa na New Zealand, Finland, Sweden na Norway, zote kwa mara nyingine tena zikiwa katika tabaka la nchi tano za kwanza aktika faharasa ya rushwa.
Infografik Korruptionsindex 2014 Englisch  
Faharasa kuhusu rushwa ya mwaka 2014

Ukraine ilipata pointi 26 na kubakia kuwa nchi inayoongoza kwa kiwango kikubwa cha rushwa barani Ulaya. Italia,Ugiriki na Romania kwa pamoja zimafanya vibaya miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya zikiwa na pointi 43.

Mwenyekiti wa Transparency International, José Ugaz alisema maafisa mafisadi huficha mali walizozipata kwa njia isiyo halali na kuzificha katika maeneo salama kupitia kampuni. Ugaz aidha amesema ufisadi mkubwa katika nchi zenye uchumi mkubwa haukandamizi tu haki za binadamu kwa watu masikini, bali pia husababisha matatizo ya utawala na uthabiti.

Ripoti hiyo ilizitaka nchi zinazoshika mkia katika orodha iliyochapishwa zichukue hatua madhubuti za makusudi kupambana na rushwa kwa masilahi ya umma. Ugaz aliyataka mataifa yanayoshika nafasi za juu katika faharasa hiyo yasieneze vitendo vya ufisadi katika nchi ambazo hazijaendelea.
Shirika la Transparency International liliuhimiza Umoja wa Ulaya, Marekani na kundi la G20 la mataifa yaliyostawi na yanayoinukia kiuchumi, kuiga mfano wa Denmark na kuanzisha daftari la umma linalojumuisha tarifa muhimu za wamiliki kwa kampuni zote zilizoshirikishwa.

HUYU DIAMOND PLATNAMZ TAYARI AMEISHIKA AFRIKA HIVI HIVI KIUTANI UTANI


Post Ya Msanii AKA Kuhusu Mapokezi Ya Diamond Tanzania.

By 
Aka
AKA ni miongoni  mwa rappers wakali Africa ambaye hivi karibuni alikuwa South Africa na alishinda tuzo moja ya Channel O  ambako pia Diamond alikuwepo huko. Aka ame Repost video ya mapokezi ya Diamond iliyowekwa Sammisago.com na Kwenye Instagram ya Sammisago huku akiweka huu ujumbe.
Diamond lands back in Tanzania after winning 3 Channel O Awards and this happens … Imagine South Africans felt like this about their own artists … In my country this is something reserved for the Bieber’s and Breezy’s … Where is our pride? Where is our passion? Anyways … BIG UP DIAMOND.
aka 2 Aka

Tuesday, November 18, 2014

Polisi wa kike waelezwa kudhalilishwa kufanyiwa kipimo cha bikira



  • Bikira ni kigezo muhimu katika kujiunga na jeshi la Polisi la nchi hiyo.


 
Serikali ya Indonesia inaelezwa kuruhusu kuwafanyia wanawake wanaotaka kujiunga na Jeshi la Polisi kipimo cha bikira ,shirika la Human rights Watch limeeleza.
Shirika hilo uangalizi wa haki za binaadam liliwahoji Polisi wanawake na wanaotaka kujiunga na Jeshi la polisi ambao tayari wamepimwa katika miji sita ya nchini Indonesia,wawili kati yao wamefanyiwa kipimo hicho mwaka huu.

Monday, November 17, 2014

LESOTHO WAPIGA HATUA KATIKA HILI, TANZANIA TUNABAKI WAPI KURUHUSU "LIVE COVERAGE" VYOMBO VYA HABARI MAHAKANI?



ACCESS TO INFORMATION, FREEDOM OF EXPRESSION ,AVOID PRESS FREEDOM VIOLATION

Ni mdogo mdogo mpaka wataipata haki kamili wana habari wa Lesotho pamoja na Vyombo vyote vy habari nchini humo, Imeanza television ya Taifa ,then na vingine vitafuata. Tukumbuke pia Kenya nao walishawahi kufanya kitu kama hiki miezi kadhaa iliyopita. Isome hapo chini kwa lugha ya Kiingereza.
Media Regulation

Lesotho Television, a State television broadcaster run under the Lesotho National Broadcasting Service, was allowed to broadcast brief coverage, for the first time, of a High Court case.

Justice T’seliso Monaphathi permitted the television cameraman to take shots just minutes before he presided over a fraud case involving Lesotho’s former Minister of Finance Timothy Thahane. He is accused of defrauding the Government of Lesotho of over M18 million (equivalent of over R18 million) for an unauthorised vegetable farm in his home area.

This development gives hope to the media in that according to the High Court Act 1978 the judge has the power to order everyone to clear the court if he finds it fit. In the history of court proceedings in Lesotho television has never before been allowed to cover court proceedings. 

Friday, November 14, 2014

MSIMAMAO WA LIGI ZA SOKA TANZANIA



Vodacom Premier League
Season: 2014-2015

Table

Pos   Team Pld W T L GoalsDiff Pts
1 Mtibwa Sugar 7 4 3 0 107 15
2 Young Africans 7 4 1 2 94 13
3 Azam 7 4 1 2 84 13
4 Coastal Union 7 3 2 2 92 11
5 Kagera Sugar 7 2 4 1 62 10
6 JKT Ruvu 7 3 1 3 70 10
7 Simba 7 1 6 0 71 9
8 Polisi Morogoro 7 2 3 2 6-1 9
9 Mgambo JKT 7 3 0 4 4-3 9
10 Stand United 7 2 3 2 5-4 9
11 Ruvu Shooting 7 2 1 4 4-3 7
12 Prisons 7 1 3 3 6-1 6
13 Ndanda 7 2 0 5 8-4 6
14 Mbeya City 7 1 2 4 2-4 5

First Division League-Group A
Season: 2014-2015

Table

Pos   Team Pld W T L GoalsDiff Pts
1 Majimaji 10 6 3 1 14:77 21
2 Friends Rangers 9 5 4 0 11:56 19
3 Kimondo 10 5 1 4 12:84 16
4 Kurugenzi 10 4 4 2 12:93 16
5 Lipuli 7 4 2 1 6:33 14
6 Polisi Dar 8 3 3 2 9:63 12
7 African Sports 9 3 2 4 7:10-3 11
8 JKT Mlale 10 2 4 4 7:8-1 10
9 Ashanti United 8 3 0 5 7:12-5 9
10 Villa Squad 8 2 2 4 6:10-4 8
11 Tessema 7 2 0 5 2:9-7 6
12 African Lyon 10 1 1 8 8:14-6 4

First Division League-Group B
Season: 2014-2015

Table

Pos   Team Pld W T L GoalsDiff Pts
1 Toto African 10 7 1 2 169 22
2 Mwadui 8 4 3 1 128 15
3 Polisi Tabora 8 4 3 1 74 15
4 JKT Oljoro 9 4 3 2 123 15
5 Rhino Rangers 8 2 5 1 50 11
6 Polisi Mara 8 3 2 3 7-3 11
7 Kanembwa JKT 8 3 1 4 5-1 10
8 Polisi Dodoma 7 2 2 3 4-4 8
9 Panone 8 1 5 2 5-2 8
10 Geita 8 2 1 5 5-4 7
11 Bukinafaso 8 0 4 4 4-4 4
12 Green Warriors 6 0 2 4 2-6 2

HII NI STORI NINAYOSHARE NA WEWE KUTOKA BBC SWAHILI

watoto waongea lugha mpya isiyojulikana
Watoto wakiwa wamekaa na mamayao wakila chakula.nchini Uganda, watoto watatu waliofungiwa na baba   yao kwa miaka saba wameanza kuzungumza lugha isiofahamika
 
Watoto watatu kutoka kijiji cha Barca katika kaunti ndogo ya Aber Wilayani Oyam nchini Uganda wameanza kuzungumza lugha tofauti isiojulikana baada ya kufungiwa katika nyumba kwa miaka saba.
Lugha hiyo mpya imetajwa kuwa Leb -adam ikimaanisha lugha ya ubongo na jamii ya eneo hilo.
Inadaiwa kuwa baba ya watoto hao aliwafungia ili kuwalinda kutokana na hatari yoyote.
Kulingana ma gazeti la the monitor nchini Uganda,watoto hao hawajaathirika kiakili lakini hawawezi kuzungumza na watu wengine.Wanaamini tu kile baba yao anachowaambia.
Kulingana na mama yao watoto hao waliweza kuishi kwa kula mayai ya chura yaliochemshwa na majani,ambayo hula kila asubuhi na jioni na hutumia maji kutoka shimo lililochimbwa na baba yao.
Mama yao anasema kuwa baba ya watoto hao alimzuia kutozungumza nao hatua iliowafanya kutojifunza lugha ya kiluo wakati walipokuwa wadogo.
Mwanamke huyo amesema kuwa alionywa na baba huyo kutosema chochote kuhusu watoto hao

Friday, October 31, 2014

Kiwango cha kalori katika pombe kitajwe

Wataka pombe ionyeshe kiwango cha kalori kupunguza vitambi na unene wa kupitiliza

Pombe inatakiwa kuwa na nembo inayoonyesha kiwango cha kalori au kipimo cha joto litolewalo na chakula ili kupunguza vitambi au unene wa kupita kiasi.
Madaktari wa afya ya umma, wameonya kuwa glasi kubwa ya mvinyo inaweza kuwa na kiasi cha kalori 200- sawa na donati, aina ya maandazi.
Hata hivyo idadi kubwa ya watu hawajui madhara ya kula kiwango kikubwa cha kalori.

Waziri wa Afya Jane Ellison amesema "hatua kubwa" imefanyika kwa kuviwekea nembo vyakula, na kwa suala hilo serikali italiangalia.
Sekta ya vinywaji imesema imesema iko tayari kwa wazo hilo la kuweka nembo zenye kuonyesha kiasi cha kalori, lakini kuweka nembo zinazonyesha kiwango cha kilevi katika kinywaji ni muhimu zaidi.

Sunday, October 19, 2014

Maji ya kuosha wafu,kivutio cha biashara


mortuary

Katika tukio la kushangaza na la kutaka kujiongezea mapato pamoja na kushamiri kwa biashara,wafanyibiashara wawili katika mtaa wa Lobengula nchini Zimbabwe walizozania maji machafu yanayopatikana baada ya kuosha wafu ambayo huyatumia kuvutia wateja.
Kwa mujibu wa BBC, Wawili hao waliojulikana kama ViolaTshuma na Molene Hadebe walikabiliana vilivyo baada ya Hadebe kuchukua kiwango kikubwa cha maji hayo ya kuosha maiti kabla ya mwenzake kuwasili.
Wafanyibiashara hao wanaodaiwa kuwa rafiki wakubwa walipata maji hayo kutoka chumba kimoja cha mazishi katika mji wa Bulawayo kwa biashara yao ya kila siku.
Kulingana na wafanyibiashara wengine maji hayo huuzwa kwa wafanyibishara na wanawake wanaotumia kufanya tambiko.
Maji hayo pia hutumika kuwazima wanaume walio wakali kwa wake zao baada ya kubaini kwamba wake hao wanawanyemelea wanaume wengine.
Wafanyibiashara waliohijiwa pia walibaini kuwa maji hayo pia hutumiwa kuosha matunda na hata nyanya ili kuwavutia wateja wengi kama wale wanaouhudhuria mazishi.

Wakatoliki wakataa kuwatambua mashoga.



Ndoa ya mashoga

Makundi ya kikatoliki yanayopigania haki za wapenzi wa jinsia moja yameelezea ghadhabu yao kutokana na hatua ya maaskofu wa kanisa hilo ya kukataa mapendekezo ya kutangaza msimamo kuhusu mashoga, wasagaji pamoja na watu waliotalakiana na wanaoana.
Wakati wa kumalizika kwa mkutano wa maaskofu wa kanisa katoliki, Vatican ilishindwa kupata theluthi mbili ya kura za maskofu wa kuunga mkono maoni yao kuhusu masuala hayo.
Kundi la kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja nchini Marekani la New Ways Ministry limesema kuwa hatua ya maskofu hao kuamua kujadili suala hilo ni matumaini ya siku za usoni.
Masuala hayo yanatarajiwa kuzungumziwa tena baada ya mwaka mmoja.*BBC Swahili*

Hizi ni nukuu za mapenzi kutoka kwa watu maarufu duniani october 19, 2014


Bob Marley

“Only once in your life, I truly believe, you find someone who can completely turn your world around. You tell them things that you’ve never shared with another soul and they absorb everything you say and actually want to hear more. You share hopes for the future, dreams that will never come true, goals that were never achieved and the many disappointments life has thrown at you.

 When something wonderful happens, you can’t wait to tell them about it, knowing they will share in your excitement. They are not embarrassed to cry with you when you are hurting or laugh with you when you make a fool of yourself. Never do they hurt your feelings or make you feel like you are not good enough, but rather they build you up and show you the things about yourself that make you special and even beautiful. There is never any pressure, jealousy or competition but only a quiet calmness when they are around. You can be yourself and not worry about what they will think of you because they love you for who you are. 

Friday, October 17, 2014

Hiki ndicho kilichowahi kutokea katika tarehe kama ya leo octoba 17, miaka mingi iliyopita

History logo
Miaka 41 iliyopita katika siku kama hii ya leo nchi za Kiarabu zinazouza nje mafuta zilianza kutekeleza vikwazo vya mafuta dhidi ya Marekani, Uingereza na makampuni yanayouuzia mafuta utawala wa Kizayuni wa Israel. Hatua hiyo ilichukuliwa kutokana na uungaji mkono mkubwa wa Marekani na Uingereza kwa utawala ghasibu wa Israel katika vita vya Israel dhidi ya Syria na Misri. Hatua hiyo ilipandisha sana bei ya mafuta katika masoko ya kimataifa na kutoa pigo kubwa kwa nchi hizo za Magharibi. Muda mfupi baadaye nchi za Kiarabu zilikiuka vikwazo hivyo vya mafuta na kuanza tena kuiuzia mafuta Marekani na Uingereza. Vikwazo hivyo vilionesha kuwa nchi za Kiislamu zina silaha muhimu inayoweza kutumiwa dhidi ya uungaji mkono mkubwa wa nchi za Magharibi kwa utawala katili wa Israel.

Na Siku kama ya leo miaka 31 iliyopita, aliaga dunia mtaalamu wa masuala ya jamii wa Kifaransa kwa jina la Raymond Aron. Aron alizaliwa mwaka 1905. Msomi huyo wa Kifaransa alikuwa akifundisha pia taaluma hiyo ya masuala ya jamii katika Chuo Kikuu cha Sorbonne, Paris kwa miaka kadhaa. Vilevile alikuwa akiandika makala katika majarida ya Le Figaro na Express mjini Paris. Raymond Aron ameandika vitabu vingi na hapa tunaweza kuashiria vitabu vyake vichache alivyovipa majina ya "Kuanza Vita vya Nyuklia, "Mapambano ya Kitabaka" na "Miaka ya Mwishoni mwa Karne".

Who Will Sing the Song? The 144000 of Revelation 14


An Amazing FactAn Amazing Fact
During the Gulf War, a small team of U.S. Navy SEALS created a diversion so convincing that it completely fooled the Iraqi army. About a dozen SEALS stormed the beaches of Kuwait and created such havoc that Iraqi generals believed the U.S.-led attack was coming from the sea. Iraq sent the majority of their army to repel this fake attack—only to find they had been duped as the main U.S. force came through the Saudi Arabian desert! Within hours the war was over, and it all started with less than 20 soldiers!

Each branch of the U.S. armed services has one or more elite teams of commandos that fight using covert guerrilla warfare tactics during special combat situations. To serve in one of these select units, a soldier must be highly disciplined and pass through incredibly difficult physical and mental training. Only those who demonstrate unflinching self control and perfect obedience qualify. These Special Forces commandos are given dangerous and complex missions; they rapidly attack enemy troops and raid behind enemy lines to clear the way for the main attacking force. Even a small team of these commandos, because of their intense training, can achieve great victories—defeating entire columns in short time.

Hizi ni nukuu mbali mbali zinazohusu maisha, zilizowahi kusemwa na watu maarufu duniani

“Don't cry because it's over, smile because it happened.” 
― Dr. Seuss

“I'm selfish, impatient and a little insecure. I make mistakes, I am out of control and at times hard to handle. But if you can't handle me at my worst, then you sure as hell don't deserve me at my best.” 
― Marilyn Monroe

“You only live once, but if you do it right, once is enough.” 
― Mae West

“There are only two ways to live your life. One is as though nothing is a miracle. The other is as though everything is a miracle.” 
― Albert Einstein

“This life is what you make it. No matter what, you're going to mess up sometimes, it's a universal truth. But the good part is you get to decide how you're going to mess it up. Girls will be your friends - they'll act like it anyway. But just remember, some come, some go. The ones that stay with you through everything - they're your true best friends. Don't let go of them. Also remember, sisters make the best friends in the world. As for lovers, well, they'll come and go too. And baby, I hate to say it, most of them - actually pretty much all of them are going to break your heart, but you can't give up because if you give up, you'll never find your soul mate. You'll never find that half who makes you whole and that goes for everything. Just because you fail once, doesn't mean you're gonna fail at everything. Keep trying, hold on, and always, always, always believe in yourself, because if you don't, then who will, sweetie? So keep your head high, keep your chin up, and most importantly, keep smiling, because life's a beautiful thing and there's so much to smile about.” 
― Marilyn Monroe

Ebola:Annan akosoa mataifa ya Magharibi


Annan anasema hajaridhishwa na juhudi za mataifa ya magharibi kupambana na Ebola

Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan amekosoa ambavyo mataifa ya magharibi yameshughulikia janga la Ebola.
Bwana Annan ameambia BBC kwamba hajaridhishwa kamwe na hatua za mataifa ya magharibi kupambana na Ebola.
''Ikiwa janga hilo lingekuwa limeathiri eneo lengine , hatua ambazo zingechukuliwa zingekuwa toifauti sana.''

Wakili asema Pistorius 'amefilisika'


Inaarifiwa Pistorius ametumia pesa zake kwa kesi inayomkabili
Pistorius aliangua kilio wakili wake alipoambia mahakama kuwa amefilisika


Mahakama inayosikiliza kesi dhidi ya mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini, Oscar Pistorius imeambiwa kuwa mwanariadha huyo amefilisika.
Hili lesemekana huku pande zote kwenye kesi zikitoa kauli yao ya mwisho kabla ya mahakama kutoa hukumu dhidi ya mwanariadha huyo.
Pistorius alipatikana na hatia ya mauji ya mpenzi wake Reeva Steenkamp bila ya kukusudia mwaka jana.
Jaji Thokozile Masipa anatarajiwa kutoa hukumu dhidi ya Pistorius Jumanne.
Anakabiliwa na kifungo cha miaka 15 lakini jaji anaweza kuamua kumpa kifungo cha nje au hata kumtoza faini.
Jaji ataanza kusoma hukumu Jumatatu na upande wa mashitaka unataka Pistorius apewe adhabu kubwa kuambatana na kosa lake.
Lakini mawakili wa Pistorius wameteta wakisema anapaswa kupewa adhabu ndogo kama vile huduma kwa jamii.
Wanadai kuwa mwanariadha huyo huenda akateswa akiwa jela, hoja ambayo imepingwa vikali na mkuu wa magereza.
Pistorius aliangua kilio wakli wake aliposema kuwa pesa zake zimekwisha baada ya kesi yake kufanya kwa mirzi saba.
"sio tu kwamba hana pesa bali anahisi hana tena matumaini,'' alisema wakili wa Pistorius.
Hii ni kesi yake ya kwanza. Nini kimtendekea mwanamume huyu? Nyota yake ilikuwa inaanza kung'ara,'' aliongeza bwana Roux.
Wakili alimuomba jaji kumuonea huruma Pistorius wakati atakapotoa hukumu.
Mnamo siku ya Ijumaa, kiongozi wa mashitaka alikosoa pendekezo la Pistorius kuikabidhi familia ya Reeva pesa. Hata hivyo familia ya Reeva ilikataa pesa hizo ikisema ni pesa za uovu.
Bwana Nel pia alisema ikiwa Pistorius atapewa adhabu ya kiungo cha nje na kuamrishwa kuihudumia jamii, itakuwa ni hujuma kwai adhabu hiyo itakuwa ndogo sana kulingana na kosa lake.

Sunday, October 12, 2014

Vichwa vya habari magazeti ya leo October 12

.
.
.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
,
,
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
DSC04138
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.