Monday, December 21, 2015

Upasuaji kwa njia ya Roboti




Hospitali moja katika manispaa ya Chongqing nchini China imefaulu kutumia roboti kufanya upasuaji wa kutoa uvimbe kutoka mwili wa mgonjwa wa saratani ya kongosho.Hospitali hiyo imesema kuwa huo ulikuwa upasuaji wa kwanza wa aina hiyo kuwahi fanywa na roboti kote duniani.


Thursday, December 17, 2015

Maelfu waandamana kupinga utawala wa Zuma


Maelfu ya watu wameandamana katika miji mikuu ya Afrika Kusini wakitaka kutimuliwa kwa Rais Jacob Zuma kwa madai kuwa visa vya ufisadi na mapendeleo vimeongezeka sana.

Makundi yaliyoandaa maandamano hayo yamekuwa yakitumia kitambulisha mada #zumamustfall kutafuta uungwaji mkono mtandaoni.
Maandamano hayo yamefanyika Siku ya Maridhiano, siku ya mapumziko ambayo lengo lake ni kuleta pamoja watu wa asili mbalimbali Afrika Kusini.
Zuma
Mwandishi wa BBC Karen Allen aliye nchini humo anasema

Video ya dk 4 ikimuonesha Balozi Ombeni Sefue akizungumzia kutenguliwa kwa Dr.Hosea TAKUKURU

SOURCE: MICHUZI BLOG

Wednesday, December 16, 2015

Magufuli amfuta mkuu wa kupambana na rushwa Dr.Edward Hosea



MagufuliIma














Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Dkt Edward Hoseah, na pia akawasimamisha kazi maafisa wa nne wa taasisi hiyo.
Rais Magufuli amesema hajaridhishwa "na namna taasisi hiyo ilivyokua ikitekeleza wajibu wake katika kukabiliana na rushwa hususani kwenye upotevu wa mapato ya serikali katika bandari ya Dar es salaam.”
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue amesema Dkt Magufuli amemteua aliyekuwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru Bw Valentino Mlowola kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru.
Kwa mujibu wa Bw Sefue, Dkt Magufuli amechukua hatua hiyo baada ya kujiridhisha kuwa "utendaji kazi wa Takukuru chini ya Dkt Edward Hoseah hauwezi kuendana na kazi anayoitaka”.
Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi mara moja kwa watumishi waandamizi wanne wa Takukuru ambao walisafiri nje ya nchi licha ya Rais Magufuli kupiga marufuku safari za nje kwa watumishi wa umma.
Watumishi hao ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nikitas ambao walisafiri nje ya nchi licha ya kunyimwa kibali cha safari kutoka kwa Rais ama Katibu Mkuu Kiongozi.
Bw Sefue amesema atakayekiuka agizo la rais "atachukuliwa hatua kali”.
source: BBC swahili

Wednesday, November 25, 2015

Kama wewe unatafuta ajira, taarifa hii kutoka Secretariate ya Ajira na Utumishi wa Umma Tanzania Inakuhusu

Maelekezo muhimu ya ujazaji wa Taarifa kwenye mfumo wa Recruitment Portal kwa waombaji kazi


 Sekretarieti ya ajira katika utumishi wa Umma imeanzisha mfumo wa kielektroniki wa utumaji wa maombi ya kazi (Recruitment Portal) ambao humsaidia muombaji kazi kutuma maombi hayo popote alipo ndani na nje ya Nchi kwa njia ya mtandao.
Ni muhimu kuzingatia kuwa kabla ya ujazaji wa taarifa kwenye mfumo wa ajira kila muombaji kazi lazima awe na barua pepe ambayo ni hai(Active email address) ambayo atatakiwa kujisajili katika sehemu iliyoandikwa Register katika ukurasa wa mbele wa mfumo (Home page) kabla ya muombaji kujaza taarifa zake katika vipengele 11 vilivyoelezewa kwenye makala haya. Pia kwa waombaji wote wanatakiwa kuhakikisha taarifa zao zote wanazojaza ni za uhakika na zipo katika ukamilifu.
 
Mfumo huu unapatikana kupitia anuani ya portal.ajira.go.tz ambapo baada ya usajili mwombaji kazi atajaza taarifa zake. Mgawanyo wa taarifa hizo upo katika vipengele vikuu 11 ambavyo ni Taarifa binafsi (Personal Details), Taarifa za Mawasiliano (Contact Details), Sifa za kielimu (Academic Qualifications), Sifa za Kitaaluma (Professional Qualifications), uwezo wa lugha (Language Proficiency), uzoefu wa kazi (Working Experience), Mafunzo, Warsha na Makongamano aliyowahi kuhudhuria (Training & Workshop Attended), ujuzi wa matumizi ya kompyuta (Computer Literacy), wadhamini (Referees), viambatanisho vingine (Other Attachments) na udhibitisho wa taarifa zilizoingizwa (Declaration). Aidha kila kipengele kinapaswa kujazwa kulingana na kinavyojieleza kwa ukamilifu wake.
Kwa kuwa kumekuwa na changamoto kwa baadhi ya waombaji kazi kutojaza taarifa zao kikamilifu au kujaza baadhi ya taarifa zao kwenye vipengele visivyohusika, makala hii itajikita katika kuelezea kwa kina taarifa gani zinapaswa kujazwa kwa kila kipengele ili kuweka uelewa mpana kwa waombaji kazi kutokana na changamoto ambazo zimekua zikijitokeza kwa baadhi ya waombaji kazi kutozingatia masharti ya ujazaji wa taarifa hizo kikamilifu kwa kila kipengele kabla ya kutuma maombi ya kazi.  
Wapo baadhi ya waombaji kazi ambao wamekuwa wakijaza taarifa ambazo hazihusiani na kipengele husika hali inayoleta changamoto katika uchambuzi wa taarifa zao kwenye mfumo. Kwa kuzingatia changamoto hiyo na ili kukuza uelewa zaidi kwa waombaji kazi kupitia mfumo huo, yafuatayo ni maelezo muhimu yanayotakiwa kujazwa kwa kila kipengele kilichopo kwenye mfumo.

Tuesday, November 24, 2015

Pic of the Day

Mshindi wa ‪#‎AirtelTRACEMusicStar‬ @Mayungaa akiwa na @AKON 
nchini Marekani ambapo ameenda kwa ajiri ya kurekodi single moja 
na Star huyo wa Ghetto.

Mitandao ya Kijamii Kenya na Rais Magufuli wa Tanzania


Uchapakazi wa Rais Dkt John Magufuli unatuma ujumbe si kwa maafisa wa Tanzania pekee, bali na nchi za jirani pia na kuwaacha viongozi wa nchi hizo kwenye wakati mgumu. Kenya ambayo imekuwa ikifuatilia siasa za Tanzania tangu wakati wa kampeni, imeonesha kupenda mbinu za Magufuli na wananchi wake wanatamani mtu kama yeye.



Kwa kipindi kifupi alichoingia madarakani, Magufuli amefanya mambo makubwa na wananchi wamependa.
Ziara yake ya kushtukiza kwenye hospitali ya Muhimbili ilifichua uovu mwingi na kupelekea kufutwa kwa bodi ya wakurugenzi wa hospitali hiyo na kumuondoa Kaimu Mkurugenzi wake, Dk Hussein Kidanto. Ili kupunguza matumizi makubwa ya fedha za serikali kwaajili ya kugharamia safari za nje za viongozi wa nchi, Magufuli aliamua kuzisitisha mara moja. Dkt Magufuli pia alielekeza kiasi cha shilingi milioni 225 zilichangwa kwaajili ya kugharamia hafla ya wabunge kupongezana mjini Dodoma 

zipelekwe kwenda kununua vitanda. Badala yake shilingi milioni 15 pekee zilitumika kwaajili ya sherehe hiyo.



Siku chache baadaye vitanda hivyo na vifaa vingine vilinunuliwa na kupelekwa Muhimbili. Jumatatu hii Magufuli alitangaza kuondoa sherehe za maadhimisho ya siku ya Uhuru 
December 9 na fedha za maandalizi hayo zitumike kwa mambo mengine muhimu. Hayo na mambo mengine yamefanya Dkt Magufuli atrend nchini Kenya. 

Hizi ni baadhi ya tweets za wakenya: 

Tuesday, September 8, 2015

Kenya yaanzisha operesheni kuzima Alshabab

Rais Kenyatta amemuagiza inspekta mkuu wa polisi kuendesha operesheni dhidi ya ugaidi.


Operesheni hiyo inayoendeshwa na vikosi maalum vya kupambana na ugaidi kwa ushirikiano na jeshi la taifa linalenga wapiganaji takriban mia tatu wa Jeysh al Ayman wanaosadikika kujificha katika msitu huo. Kundi hilo la Jeysh al Ayman linasadikiwa kuwa na uhusiano na wapiganaji wa Al Shabaab

Sunday, September 6, 2015

RAMSEY NOAH: Mimi na Siasa mbalimbali


Wakati wimbi la kisiasa likiwachukua wasanii wengi wa Tanzania kutoka tasnia ya muziki na wale wa maigizo( Bongo Movie), nchini Nigeria imekuwa tofauti kwa msanii wa maigizo nchini humo Ramsey Noah, ambaye pia ni staa wa movie ya Kibongo The Devil Kingdom aliyoshirikishwa na Marehemu Stevene Kanumba. Akizungumza na mtandao wa NET Nouah amekaririwa akisema kuwa

RAMSEYNOAHINTERVIEW
yuko tofauti kabisa na wasanii wenzake wa nchini humo wanaokimbilia kwenye siasa kila kukicha na kuongeza kuwa mashabiki wake wasitegemee Ramsey kujiunga na siasa.
Akifanyiwa mahojiano maalum na mtandao wa NET wa nchini humo, Ramsey alisema kuwa: ‘Sijui jinsi gani naweza kuwa mwanasiasa, mimi sio mwanadiplomasia kivile. Sijui namna ya kuyapangilia maneno yakafana kama wanasiasa wanavyoweza kufanya. Mimi siko hivyo’.
Source: NaijaGists.com

ACACIA Yaidhamini Stendi United kwa Kitita cha shilingi bilioni moja


Kampuni ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ya Acacia iliingia mkataba wa miaka miwili na timu ya Stend United ya Mkoani Shinyanga kwa ajili ya kushiriki ligi kuu ya Vodacom ambayo inategemewa kuanza tutimua vumbi katikati ya mwezi huu. Stand United ni moja kati ya timu bora kabisa katika kanda ya ziwa ambayo imeshiriki katika ligi kuu msimu uliopita 2014/2015 na kumaliza ikiwa nafasi ya tisa.
 

Mwenyekiti wa stand united Amani Vicent (kushoto) akibadilishana mkataba wa udhamini wa timu hiyo na Makamu wa rais wa ACACIA anaeshugulikia masuala ya Kampuni, Deo Mwanyika mara baada ya kutiliana saini mkataba wa miaka miwili na kampuni hiyo.

Al Shabab wateka miji miwili kusini mwa Somalia

 http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/fec01bb37336bdc554b56465a0fd13d5_XL.jpg
Magaidi wa kundi la al Shabab wamedai kuchukua udhibiti wa miji miwili kusini magharibi mwa Somalia siku chache tu baada ya kushambulia kituo cha vikosi vya Umoja wa Afrika katika eneo hilo.
Msemaji wa al Shabab amesema kundi hilo limeteka miji miwili midogo katika eneo la Lower Shabelle ambayo ni El Saliindi, yapata kilomita 65 kusini mwa Mogadishu na Kuntuwarey katika barabara ya Mogadishiu-Barawe.

Saturday, September 5, 2015

Hivi ndivo Juan Cuadrado alivofanyiwa na Shabiki wa Juventus kwa Mapenzi mema


Winga wa kimataifa wa Colombia na klabu ya Chelsea  Juan Cuadrado ambaye kwa sasa anacheza kwa mkopo katika klabu ya Juventus ya Italia, shabiki wake kafanya jambo hili la kuvutia baada ya kufurahishwa na ujio wa winga huyo katika klabu ya Juventus, hivyo kanyoa nywele kwa style ya picha ya Juan Cuadrado.
COAFg_rVEAI8OmS
Juan Cuadrado alijiunga na klabu ya Chelsea kwa ada ya uhamisho wa pound milioni 27 pamoja na bonus akitokea klabu ya Fiorentina ya Italia ila amejiunga na Juventus kwa mkopo baada ya kukosa nafasi ya kucheza kikosi cha kwanza kwa mabingwa hao wa Uingereza.
SOURCE: Millard ayo

MwanaHalisi yaachiwa Huru-

Toleo la gazeti la MwanaHALISI lililosababisha kufungiwa
MAHAKAMA Kuu ya Tanzania imesema Waziri wa Habari, Dk. Fennela Mkangara hakufuata utaratibu wa kisheria katika kulifungia gazeti la MwanaHALISI Julai 30 miaka mitatu iliyopita. Anaandika Erasto Stanslaus … (endelea).

Diamond Platnumz atwaa Tuzo nchini Uganda


Kushoto ni tuzo aliyochukua Diamond Platnumz.
MKALI wa Bongo Fleva nchini, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' ametwaa tuzo ya Msanii Bora wa Afrika katika tuzo zilizotolewa na Uganda Entertainment. Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Diamond amewashukuru mashabiki wake waliompigia kura na kufanikiwa kutwaa tuzo hiyo pamoja na kuwaomba waendelee kumpigia kura katika vipengele vingine ambavyo anawania tuzo mbalimbali.

Diamond Platnumz.
Alichokiandika Diamond baada ya ushindi huo: SOURCE: Mjengwa blog


Mashehe 6 waliotekwa DRC wazungumza yaliyowasibu baada ya kurudi nchini


Ebola yatatiza tena Sierra Leone


Watu 1,000 nchini Sierra Leone wamewekwa kwenye karantini baada ya kugunduliwa kuwa mwanamke wa umri wa miaka 67 alifariki kutokana na Ebola.
Hilo limejiri siku tano tu baada ya kuanza kwa hesabu ya wiki sita iliyolenga kutangaza taifa hilo kuwa bila Ebola.

 Maafisa wa kukabili Ebola

Putin: Sera mbovu za Ulaya, sababu ya mgogoro wa wahajiri'


 
Rais Vladmir Putin wa Russia amesema leo kuwa, mgogoro wa wahajiri unaolikabili bara Ulaya kwa sasa umetokana na sera mbovu za kigeni za nchi za bara hilo hususan zile ambazo ni wanachama wa Umoja wa Ulaya (EU). Kiongozi huyo amesisitiza kuwa, uingiliaji wa Wamagharibi katika mambo ya ndani nchi za Mashariki ya Kati na kaskazini mwa Afrika ni moja ya sababu za kuibuka mgogoro wa wahajiri katika nchi za EU.

Kikwete: Uwajibikaji utasaidia maendeleo ya Afrika

    kuzisha hati

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema mapema leo kuwa, uwazi na uwajibikaji utasaidia kuharakisha maendeleo barani Afrika. Rais Kikwete amesema hayo wakati wa kufungua rasmi mkutano wa takwimu huria barani Afrika ulioanza leo jijini Dar es Salaam. Kwenye hotuba yake Rais Kikwete amesema kuwa, serikali za Afrika zinapaswa kuweka wazi takwimu zao ili raia wawe na ufahamu wa yale yanayofanywa na viongozi wao. Rais wa Tanzania amesema kufanya hivyo kutaondoa misuguano inayoshuhudiwa mara kwa mara kati ya raia na serikali hususan nyakati za matukio ya kisiasa kama vile uchaguzi mkuu au kura ya maamuzi.
Mkutano huo wa siku mbili unahudhuriwa na zaidi ya wajumbe 400 kutoka nchi kadhaa za Afrika wakiwemo wawakilishi wa serikali, sekta binafsi, wataalamu na wasomi pamoja na wawekezaji.
SOURCE: TEHRAN

Monday, June 22, 2015

Jaji Warioba asema kitu juu ya wagombea urais CCM


Dar es Salaam. Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amewashangaa makada wanaojinadi kuwa ni wasafi na waadilifu, akisema sifa hizo zinatakiwa zitolewe na jamii.
Jaji Warioba, mmoja wa watu ambao wamekuwa wakikemea masuala ya ukiukwaji wa maadili, pia amesema hatamuunga mkono mgombea ambaye anakiuka maadili ya uongozi.
Tayari makada 37 wamejitokeza kuomba ridhaa ya wana-CCM kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na wengi wao wamekuwa wakijinadi kuwa ni wasafi na waadilifu na kuwataka wanachama kutowapitisha watu wenye harufu ya ufisadi na wasio waadilifu.
Lakini Jaji Warioba alisema anaona wanakwenda kinyume na inavyotakiwa kufanyika.
“Viongozi wa sasa wanaonekana hawajali misingi ya maadili kwa sababu jamii yetu yenyewe imeonyesha kutochukizwa na suala hili la mmomonyoko wa maadili na wala jamii haijalipa uzito unaostahili,” alisema Jaji Warioba wakati wa uzinduzi wa kampeni ya Vuguvugu la uhuishaji wa Maadili kwa Jamii (Moral Rivival Movement).

Usher Raymond na Justin Beiber kulipa faini kwa kukopi wimbo wa "Somebody to Love"



Justin Bieber na Usher Raymond wamekutwa na shtaka na wametakiwa kulipa Dola million 10 baada ya kukopi wimbo "Somebody to Love" iliyofanyika mwaka 2010.

Muandishi wa nyimbo anayeafahamika kama Mareio Overton na muimbaji Devin Copeland anafahamika kama De Rico, wana wimbo wenye jina kama hilo hilo na wanawashtaki kwa wizi wa jina hilo (Copyrights Violation).
Wanasema ngoma hiyo inayo saini ya wakati sawa, beat, chords sawa na mashairi kwenye wimbo wao, Reuters imeripoti.
“Baada ya kusikiliza Copeland na wimbo wa Bieber na Usher, tuna hitimisha kwamba viitikio vyao vimefanana” Jaji Pamela Harris aliiandikia mahakama ya rufani.
Kesi hiyo ilifutwa Machi 2014 na Jaji wa U.S District ambae alihisi mahakama haiwezi kuona wizi wowote uliofanyika, Lakini Harris alisema kwamba mashairi “somebody to Love” imeimbwa “sawa kabisa na melody.
Source: Mjengwa Blog

Vilabu ruksa kusajili 7 wa kigeni Ligi Kuu Tanzania Bara




Kiwango cha ushindani Ligi kuu ya Tanzania Bara kinatarajiwa kuongezeka na kufungua milango zaidi kwa wachezaji wa kigeni baada ya vilabu kuruhusiwa kusajili wachezaji 7 wa kigeni kuanzia msimu ujao wa ligi.
Awali, baadhi ya vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya Tanzania Bara vilipendekeza usajili wa wachezaji 10 wa kigeni lakini Shirikisho la mpira wa miguu (TFF) limeamua ni 7 tu wanaweza kusajiliwa na kucheza kwa wakati wote.
Katika misimu iliyopita, kila timu iliruhusiwa kusajili wachezaji wa kigeni wasiozidi watano.
Hata hivyo, si vilabu vyote vitaweza kusajili wachezaji wa kigeni kwa kuwa na vyanzo vidogo vya pesa, bali vilabu vikubwa kama vile Simba,Yanga na Azam vitaweza kumudu gharama za usajili
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TFF, mikakati ya kusajiliwa wachezaji hawa ni haya yafuatayo:
- Mchezaji awe ni mchezaji wa timu za Taifa za nchi yake kuanzia timu ya taifa au timu za vijana za U23, U20, U19 na U17.
- Mchezaji awe anacheza katika ligi kuu ya nchi yake au nchi nyingine wakati anasajiliwa.
Wimbi la wachezaji wa kigeni linaongezeka nchini Tanzania baada ya ligi ya nchi hiyo kuwa ni ligi yenye ushindani na vilabu kutoa pesa nyingi kwa ajili ya usajili na mshahara.
Kwa habari zisizo rasmi, ligi ya Tanzania Bara inasemekana ndio ligi inayoongoza katika ukanda wa Afrika ya Mashariki kwa ushindani.
Source: BBC Swahili

Mchezaji wa kigeni kulipa Tanzania



Shirikisho la soka nchini Tanzania (TFF) limepitisha azimio la kila mchezaji wa kigeni kulipa dola 2,000 ( wastani wa milioni 5) kwa kila msimu atakaocheza ligi kuu ya Tanzania.
Kiasi hicho cha pesa kitaanza kulipwa katika msimu ujao wa ligi wa 2015/2016 .
Wachezaji wa kigeni waliosalia kuendelea kuchezea timu zao na wale wanaosajiliwa kwa ajili ya msimu ujao watalazimika kulipa kiasi hicho cha pesa.
Msemaji na afisa habari wa TFF, Baraka Kizuguto amesema maamuzi ya kikao cha kamati ya utendaji ya TFF kilichoketi Jumamosi visiwani Zanzibar ni kuwa kiasi hicho cha pesa kitakuwa ni kwa ajili ya kuendeleza mpira wa miguu nchini Tanzania.
Katika miaka ya nyuma, wachezaji wa kigeni kutoka nchi mbalimbali, hasa za Afrika ya Mashariki, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi walikuwa hawatozwi kiasi chochote cha pesa licha ya kulipwa mamilioni.
Kizuguto amesema fedha hizo zitapelekwa katika mfuko wa maendeleo ya mpira wa miguu ujulikanao kama (Football Development Fund
Source: BBC Swahili

Sunday, April 26, 2015

De Gea kupewa ofa ya Paund 200,000 ili kubaki old trafford na kupewa Kipa anaelipwa fedha nyingi zaidi

de gea

David de gea amekua akihusiswa na kuhamia Real Madrid misimu huu utakavyokwisha.
Manchester united wamempa ofa ya paundi 200,000 ili abaki
Kama atasaini atakua golikipa anaelipwa zaidi duniani

Louis van Gaal alikubali ijumaa hii kwamba klabu imempa mshahara mkubwa sana.
Manchester United wametoa ofa hiyo kwa David de Gea na kumfanya gilikipa ambae analipwa zaidi duniani kama atakubali kusaini mkataba mpya ambao atakua anapokea kitita cha paund laki mbili kwa wiki.(P.T)

TIGO WAMEINGIA KATIKA HEADLINES WAZINDUA INTANETI YA KASI ZAIDI 4G LTE

Muonekano katika duka la tigo mlimani city ambapo wateja walishuhudia jinsi gani mtandao huu wa kasi wa intaneti unavyofanya kazi kwa kuona matukio laivu kwa kutumia mtandao wa intaneti Kampuni ya simu Tigo Tanzania leo imezindua teknolojia mpya ijulikanayo kama 4G LTE ambayo utaifanya kuwa  mtandao wa intaneti wenye kasi zaidi kuliko yote nchini Tanzania 

Je,miraa inaongeza nguvu za kiume?



Wanaume katika eneo la Meru mashariki mwa Kenya ambao hawana uwezo wa kuwatosheleza wake zao kupitia tendo la ngono sasa wametakiwa kutokuwa na wasiwasi.

Friday, April 24, 2015

JK AONGOZA MAZISHI YA KITENGA MKOANI MOROGORO



Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Kikwete (pichani kati) na Waziri Mkuu Mh.Mizengo Pinda (pichani shoto) wakishuhudia askari wa jeshi la Wananchi (JWTZ) wakipiga risasi hewani kama sehemu ya heshima ya kumuaga aliyekuwa mkuu wa wilaya mpya ya Kyerwa mkoani Kagera jana ,Marehemu Luteni Kanali Benedict Kitenga (mstaafu) huko kwenye makaburi ya Mlima Kola Kigurunyembe mkoani Morogoro. PICHA NA IKULU.(Muro)
source:Mjengwa

SHEREHE YA UKUZAJI WA KISWAHILI YAENDELEA WASHINGTON, DC



Rais wa CHAUKIDU Prof Lioba Moshi watatu toka kushoto akimkaribisha Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi mara tu alipowasili kama mgeni rasmi chuo kikuu cha Howard Washington, DC siku ya Alhamisi April 23, 2015 kulia ni Prof Venessa White Jackson.

Wanawake wanaokuwa watawa waongezeka UK kutoka 15 kwa mwaka hadi 45



 
 Watawa katika mkutano na kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis

Idadi ya wanawake wanaokuwa watawa imeongezeka pakubwa katika kipindi cha miaka 25,kanisa katoliki nchini Uingereza na Wales limesema.

Takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya wanawake wanaokula viapo vitakatifu imeongezeka mara tatu katika kipindi cha miaka mitano kutoka wanawake 15 mwaka 2009 hadi 45 mwaka uliopita,ikiwa ni idadi kubwa tangu mwaka 1990.

Boko Haram labadilisha jina Nigeria

Kiongozi wa wapiganaji wa Boko Haram Abubakar Shekau
Picha mpya zimetolewa kuhusu wapiganaji wa Boko Haram ambao wanajielezea kuwa Islamic State Jimbo la Magharibi mwa Afrika.

Wednesday, January 28, 2015

Kombe la mataifa ya Afrika 2015

Kundi D 
 
Cameroon vs Cote d'voire 

Guinea vs Mali

Kisa Cha Marafiki Watatu: Julius, Oscar Na Rashid..


 Ndugu zangu,

Nimeandika huko nyuma, kuwa watatu hawa, Julius Nyerere, Oscar Kambona na Rashid Kawawa, kuwa ndio walikuwa Watanganyika wenye nguvu na ushawishi mkubwa kwenye Tanganyika Huru.
Nchi ilikuwa changa, na viongozi nao walikuwa wachanga sana. Nyerere alikuwa mbele yake na dhamana kubwa aliyoibeba.
 

Nchi ilihitaji kujitambua, kisha kusonga mbele. Nyerere, mwalimu wa kawaida, ambaye hakupata hata kuwa Headmaster pale Pugu Sekondari, anaambiwa, kuwa sasa wewe ni Head Of State - Mkuu Wa Nchi.

Na wakati huo Dunia ilikuwa kwenye Vita Baridi. Iligawinyika kati ya Ubepari na Ukomunisti. Nyerere haliona, kuwa hatuwezi kuwa nchi ya kibepari, lakini, hatuwezi pia kuwa nchi ya Kikomunisti. Nyerere alialikwa Marekani, akafika China pia. Kuna mazuri aliyaona Marekani, na mazuri aliyaona China.

Sunday, January 18, 2015

JE UGUNDUZI WA KIFAA HIKI UTAWEZA KUPUNGUZA MICHEPUKO KATIKA MAHUSIANO?


Waswahili husema kwamba siku za mwizi ni arobaini. Msemo huo sasa huenda ukafanikishwa miongoni mwa akina baba ambao huenda kinyume na ndoa zao na wabakaji.

Hii ni baada ya kubuniwa kwa kifaa kwa jina Semenspy kilicho na uwezo wa kubaini majimaji yaliosalia katika chupi,nguo za kulalia,katika nguo na maeneo mengine baada ya mtu kuhusika katika tendo la ngono.

Kulingana na gazeti la the Nairobian nchini kenya,kifaa hicho pia kina mwongozo unaofanya mambo kuwa rahisi kwa wanandoa walio na shauku miongoni mwao.
Maagizo yake ni kwamba iwapo unamshuku mumeo ama mkeo tafuta majimaji hayo katika chupi ama nguo zilizotajwa hapo awali.

Kama kifaa cha kupima iwapo mwanamke ni mja mzito Semenspy kinaweza kubaini mara moja iwapo mtu ana uhusiano mwengine nje. Kulingana na daktari Wachira wa DIY Solutions, kifaa hicho kimetengezwa Marekani.Wachira amebaini kwamba amefanikiwa kupata majibu sahihi kutoka kwa wanawake wanaotaka kujua iwapo waume zao na marafiki zao wa kiume wanawadanganya katika uhusiano.

Si rahisi kuwakamata wapenzi wanaodanganya kwa kuwa kunahitaji upelelezi zaidi na subra.
kwa kuwa kuna maji maji ya mbegu za kiume katika chupi ya mwanamume sio ushahidi kwamba mwanamume huyo anakwenda nje ya ndoa.

Swali ni vile utakavyoonyesha ushahidi kwamba maji maji hayo yanatoka kwa mwanamume huyo kwa kuwa mara nyingi wengi hutoa maji hayo bila ya kuhusika katika tendo la ngono. Daktari Wachira ana shauri kwamba mwanamke anayemchunguza mumewe anafaa kukaa kwa mda bila kufanya mapenzi, ili kuweza kuchukua sampuli za maji maji hayo kutoka kwa nguo za mumewe ama mpenziwe.

Ameongeza kuwa, violezi hivyo vinafaa kuchukuliwa mara tatu na kutoka nguo tofauti za mpenzi anayeshukiwa. Aidha si kila mara kwamba maji maji ya mbegu za kiume humtoka mwanamume bila ya kufanya mapenzi kwa hivyo hiyo haifai kuwa sababu ya mwanamume kujilinda.
SOURCE: BBC 

TANGAZO LA MTIHANI KIDATO CHA NNE 2015


http://in2eastafrica.net/wp-content/uploads/2014/09/Dr-Charles-Msonde.jpg

 Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani Tanzania Dr. Charles Msonde

Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania anapenda kuwatangazia watu wote wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato Cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) Mwezi Novemba 2015 kwamba usajili umeanza rasmi tarehe 01 Januari 2015. 

Watahiniwa watakaojisajili katika kipindi cha kawaida yaani tarehe 01 Januari 2015 hadi 28 Februari 2015 watalipa ada ya Shilingi 50,000/- kwa wanaojisajili mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Shilingi 30,000/- kwa wanaojisajili mtihani wa Maarifa (QT).

Watahiniwa watakaojisajili kwa kuchelewa yaani kuanzia tarehe 01 Machi 2015 hadi tarehe 31 Machi 2015 watalipa ada ya Shilingi 65,000/ kwa Kidato cha Nne na ada ya Shilingi 40,000/- kwa mtihani wa Maarifa (ada pamoja na faini).

Waombaji wote watajisajili kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya Baraza la Mitihani: www.necta.go.tz. Kabla ya kujisajili kwenye mtandao waombaji watapaswa kwenda kwenye vituo wanavyokusudia kufanyia mtihani kuchukua namba rejea (Reference Number).

Wakuu wote wa vituo nchini wamekabidhiwa namba rejea na watazigawa kwa watahiniwa tarajali bila malipo. 

Aidha waombaji watapaswa pia kulipa ada ya mtihani kwa njia ya Posta au M-Pesa kabla ya kujisajili kwani hakuna mtahiniwa atakayeweza kujisajili bila kulipa ada ya mtihani. 

Waombaji wote wazingatie kwamba kipindi cha usajili kitafungwa rasmi tarehe 31 Machi 2015.